• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MHANDISI LUHEMEJA: USAFI WA MAZINGIRA SASA NI LAZIMA KUTOKOMEZA MAGUGU MAJI

Posted on: March 10th, 2025

MHANDISI LUHEMEJA: USAFI WA MAZINGIRA SASA NI LAZIMA KUTOKOMEZA MAGUGU MAJI


Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhandisi Cyprian Luhemeja ametoa maagizo ya kufanyika kampeni maalum ya usafi wa mazingira kwenye mialo yote inayozinguka ziwa Victoria ili kutokomeza ukuaji wa magugu maji ambayo yamezidi kushamiri ziwani humo.

Akitoa maelekezo hayo mapema leo asubuhi Machi 10, 2025 kabla ya kuanza zoezi la kukagua hali halisi ya magugu maji hayo eneo la Kigongo Wilayani Misungwi, Luhemeja amebainisha kampeni hiyo ya usafi sasa siyo ya hiari bali ya lazima na kuwataka Wakurugenzi wote wa Halmashauri kuitikia wito huo ili kuepukana na hasara za kuwepo magugu maji hayo ziwani.

"Ndugu zangu hali halisi tunaiona mbele yetu siyo nzuri, hali ya usafiri inazidi kuwa ngumu na ukuaji wa viumbe maji upo hatarini, ni lazima hatua za haraka zianze tukianzia na azimio la usafi”. Amesisitiza Mhandisi Luhemeja.

Amesema wamelazimika kuja na Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe, Mwakilishi wa Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Maji, na Viongozi wengine waandamizi kutoka Tamisemi na Makatibu Tawala wa Mikoa kutoka Kanda ya ziwa, lengo ni kukutana na kutoa jawaba la haraka kulinusuru ziwa Victoria na janga hilo.

Aidha Katibu Mkuu huyo mara baada ya kupata taarifa fupi kutoka kwa Meneja wa Kanda wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Bw. Joram Kayombo kwamba nchi ya Uganda wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokomeza magugu maji, ameagiza wataalamu kutoka nchini kwenda huko ili kupata uzoefu wa kitaaluma ili kuja kusaidia kukabiliana na hali hiyo.

Awali akiwakaribisha Ofisini kwake viongozi hao waandamizi, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema magugu maji yamekuwa tishio katika kukuza uchumi wa buluu kutokana na uwepo wake kunashusha mazalia ya viumbe maji, shida ya usafiri na ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba nao kuwa mgumu.

"Nina imani na timu hii iliyochanganyika na wataalamu tofauti na masuala ya mazingira kuja na jawabu chanya ili kuendelea kulipa uhai ziwa Victoria”. Mhe. Mtanda.

Viongozi hao waandamizi kutoka Wizara mbalimbali siku ya kesho watakutana kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa le ngo la kutoa maazimio kukabiliana na janga hilo la magugu maji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti