• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Michezo ya UMITASHUMTA yazinduliwa rasmi Mwanza

Posted on: July 20th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amewataka wanafunzi Kujituma, kuweka bidii ya kizalendo na kufuata Sheria na Taratibu za Michezo ili kupata wanamichezo bora watakaouwakilisha Mkoa kwenye michezo ya UMITASHUMTA Kitaifa Mkoani Tabora mwishoni mwa mwezi.

Ametoa wito huo leo Julai 19, 2022 wakati akifungua Michezo ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) inayowakutanisha wanafunzi 660 kutoka Halmashauri 8 za Mkoa wa Mwanza wanaoshiriki michezo hiyo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Nsumba.

"Wachezaji mliochaguliwa kushiriki michuano ya Mkoa mnapaswa kujituma ili muweze kufuzu michuano ya Mkoa, Kitaifa na hata badae ya kimataifa kwani vipaji ni ajira na biashara hivyo zingatieni yote ili mtimize ndoto zenu." Amesema.

Martin Nkwabi, Afisa Elimu Mkoa amesema kuwa kwenye mfumo wa Elimu kuna uhusiano mkubwa sana kati ya elimu na michezo na ndio maana sehemu ambayo michezo imeimarika watoto wanafaulu zaidi kwakua afya ya mwili inafungua akili vizuri zaidi.


Amefafanua kuwa michezo husaidia kufuta ubaguzi wa makabila, elimu, rangi na kufanya watu kuwa wamoja na wenye mshikamano kwani kinachozingatiwa ni umahiri tu uwanjani bila kujali ni nani ameonesha kipaji hicho.


 Joseph Mambo, Mratibu wa UMITASHUMTA Mkoa wa Mwanza 2022 amebainisha kuwa mashindano hayo ngazi ya Mkoa yatadumu kwa siku tano na watakaofuzu watauwakilisha Mkoa Kitaifa Mkoani Tabora mwishoni mwa Mwezi Julai mwaka huu.


Vilevile, amefafanua kuwa mashindano hayo muhimu yatahusisha pia wanafunzi kutoka makundi maalumu yatasaidia kuwaunganisha vijana wa Tanzania kitaifa, kupanua wigo wa ufahamu wa watoto kijiografia na kuibua vipaji na taaluma kwa watoto ni miongoni na taaluma.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti