• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MIUNDOMBINU BORA YA SHULE YAONGEZA HAMASA YA UANDIKISHAJI WANAFUNZI NYAMAGANA

Posted on: January 9th, 2024

MIUNDOMBINU BORA YA SHULE YAONGEZA HAMASA YA UANDIKISHAJI WANAFUNZI NYAMAGANA


*Uandikishaji wa wanafunzi wavuka matarajio shule za awali na msingi*


*RC Makalla amshukuru Rais Samia kwa Ujenzi wa madarasa*


*Shule mpya ya Kanenwa yawapunguzia watoto adha kutembea umbali mrefu*


*RC Makalla aagiza umeme na maji kupelekwa kwenye shule mpya*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amekagua miundombinu ya elimu ya awali, msingi na sekondari wilayani Nyamagana pamoja hali ya uandikishaji wa wanafunzi ambapo amebaini kuwa ujenzi wa miundombinu bora umepelekea uandikishaji wa wanafunzi kuvuka lengo la matarajio

Akiongea katika nyakati tofauti wilayani humo leo tarehe 09 Januari 2024, Mkuu wa Mkoa amesema matokeo ya usajili wa wanafunzi yanatokana na nia njema ya Serikali ya awamu ya sita ya kuhakikisha miundombinu kwenye shule za msingi na sekondari inaimarika ili kuwa na mazingira mazuri ya kujifunza na kujifunzia.

Kutokana na ujenzi wa shule mpya ya msingi Kanenwa Mhe. Makalla amebainisha kuwa si tu imevunja rekodi ya uandikishaji kwa wanafunzi wa awali (Maoteo 150, walioandikishwa 350) na darasa la kwanza (Maoteo 200, waliosajiliwa 250) bali itaondoa adha ya watoto kutembea umbali mrefu kwenda kwenye shule za Bujingwa na Bukaza.

"Leo ni siku ya pili tangia shule zifunguliwe, kuanzia walimu, uongozi wa kata na wilaya, wazazi na walezi nisisitize tuweke msukumo, ushawishi na ufuatiliaji wa wanafunzi waweze kuripoti shuleni." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa akiwa kwenye shule ya sekondari Mirongo ambayo wameripoti watoto 71 kati ya 223.

Vilevile, Mhe. Makalla ameongeza kuwa shule zote mpya ndani ya Mkoa huo zimesajiliwa na hali hiyo itasaidia kuwa na wigo mpana wa watoto kupata shule za jirani na akatumia wakati huo kuwaagiza TANESCO na MWAUWASA kupeleka huduma kwenye shule mpya ili kutoa fursa kwa wanafunzi na walimu kuwa na mazingira mazuri ya ujifunzaji na kufundishia.

Wakati akitoa pongezi na shukrani kwa Rais Samia kwa kuhakikisha elimu inakua bora nchini, Makalla amewapongeza uongozi wa wilaya na Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa miundombinu hususani ya madarasa ya ghorofa na kuhakikisha wanafunzi wanaripoti shuleni kwa wakati mara tu muhula mpya wa masomo ulipoanza mapema wiki hii.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mhe. Stansilaus Mabula ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe. Rais kwa kumwaga pesa nyingi kwenye uboreshaji wa miundombinu ya elimu na kuwapongeza watendaji wote ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa ushirikiano uliopelekea ukamilishaji bora wa miundombinu ya shule.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti