• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MKONO WA EID WA RAIS SAMIA WAGUSA WENYE UHITAJI MWANZA

Posted on: January 31st, 2025

MKONO WA EID WA RAIS SAMIA WAGUSA WENYE UHITAJI MWANZA


Katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al- Fitri na kutamatika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani, Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa mkono wa Eid kwa kambi ya wazee wasiojiweza na vituo viwili vya watoto yatima mkoani Mwanza.

Akiwasilisha zawadi hizo katika kambi ya wazee Bukumbi- Misungwi, Markazi ya watoto yatima ya Sharif Said Nyegezi- Nyamagana pamoja na kituo cha palezi ya watoto cha Kamanga, mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda amesema Rais Samia anaendeleza utamaduni wake wa kuwakumbuka wenye uhitaji hivyo ametoa zawadi ili kusherehekea vyema sikukuu pamoja nao

“Wanasema kinywa cha Mzee kina busara sana msiache kumuombea Rais wetu awe na afya njema ya akili ya mwili ili aweze kuliongoza vyema Taifa letu”. Amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, Mkuu wa Mkoa akiwa katika kituo cha Markazi ya Sharif Said ameahidi kuchangia kujenga darasa moja ili watoto hao waendelee kupata elimu ya dini itakayowasaidia kuitetea na kuisambaza dini.

Baadhi ya viongozi kutoka kwenye kambi ya kulelea wazee hao wamemshukuru Mhe. Rais Samia kwa kuwa na moyo wa kutoa na kulikumbuka kundi hilo ambalo nalo linatakiwa kufurahia sikukuu hizi.

Nao watoto kutoka kituo cha Markazi ya watoto yatima ya Sharif Said Nyegezi wamemshukuru Rais Samia shukrani zilizoambatana na dua maalumu ya kumuombea afya njema na umri mrefu wenye manufaa.

Jumla ya fedha zilizotolewa katika Mkoa wa Mwanza ni shilingi milioni 10 ambapo wamenunuliwa jumla ya mbuzi 12, mchele gunia 12, mafuta ndoo kubwa 12, sukari mifuko 12 na soda katoni 90.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti