• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mongella aagiza kuundwa timu itakayosimamia uvuvi,kilimo,mifugo kuongeza ufanisi

Posted on: September 20th, 2019


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella ameagiza kuundwa timu ya wajumbe watakaosaidia kusimamia sera bora ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Agizo hilo limetolewa jijini Mwanza wakati wa mkutano na wadau wa sekta hizo uliolenga kujadili hali, mwenendo na mafanikio yake kimkoa.

Timu hiyo yenye wajumbe kutoka sekta husika inatarajiwa kuandaa na kusimamia Mwongozo bora utakaosaidia wakulima, wafugaji na wavuvi kupiga hatua kiuchumi na hatimaye kuchangia pato la mkoa na taifa kwa ujumla.

"Tunaenda kuunda timu ya wajumbe watakaotusaidia kuandaa mwongozo wa njia bora za kufikia mafanikio kwenye sekta hizi na tutaweka wazi mawasiliano yao ili kama mtu ana maoni ya maboresho ya sekta hizi muhimu basi awasiliane nao na niwahakikishie tutafanyia kazi maoni ya kila mtu atakayoleta kwetu.

"Kwa hiyo kwa wenzetu mliopo kwenye nafasi ya uandaaji mbegu au uchakataji mazao yote nanyi pia fanyieni kazi mawazo ya wakulima maana wao ndio wanaelewa hali halisi, wapeni nafasi wasikilizeni na msijifanye mnajua kila kitu.

"Kama ambavyo tumekubaliana sasa ni wakati wa vitendo, tunatoka kwenye nadharia tunaenda kufanya kazi, tunataka matokeo chanya yaonekane kwa mkulima, mfugaji na mvuvi wetu.

"Muda wa kukaa tunaongea tu umekwisha, tumefanya majaribio kwenye pamba na tumeona tunao uwezo wa kusukumana tukafika, kwenye mifugo tumejitahidi lakini bado, sasa tuhamishie nguvu pia kwenye mpunga na alizeti ndani ya misimu miwili natajia kuona uzalishaji unaongezeka mara dufu", Alisema Mongela.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Usimamizi Bodi ya Pamba Tanzania, James Shimbe alisema kuwa ni wakati sasa wa kuwa na kilimo chenye tija hasa kwenye pamba, kwani ni wazi kuwa takwimu zinaonyesha uzalishaji wa mazao unaongezeka japo manufaa kwa mkulima yamebaki kuwa siyo makubwa.

" Kwa muda mrefu kilimo nchini kwetu kimeonekana hakina tija kwa sababu tumezoea kufanya uzalishaji ambao hauna tija, lakini mabadiliko tunayaona baada ya kuanza kutoa semina kwa wakulima wetu.

"Mfano msimu huu uzalishaji umeongezeka baada ya wakulima waliokuwa hawazalishi kwa tija kuwafikia na kuwapa mafunzo ya uzalishaji na uvunaji wenye tija lakini mbali na kuzalisha kwa tija hivi sasa ifikie hatua kuwe na malipo ya nyongeza ya thamani hasa kwa wakulima wanaozalisha mazao yenye thamani zaidi ya moja hasa wakulima wa pamba ambayo inatoa nguo pamoja na mafuta hivyo mnunuzi anafaidika mara mbili au zaidi kumbe na mkulima anatakiwa anufaike vivyo hivyo",Alisema Shimbe.

Naye Katibu Mkuu  wa Umoja wa Wafugaji Mkoa wa Mwanza (UWAWAMWA), Rehema Mwalugala aliiomba Serikali kutenga aridhi ya kutosha kwa ajili ya malisho ya mifugo ya kisasa na yale ya kawaida.

"Sisi kama wafugaji Mkoa wa Mwanza tupo kwenye mipango ya kuunda vikundi ili   tuweze kukopesheka kiurahisi pamoja na kukuza ushirikiano kati yetu na taasis za serikali.

"Ila niiombe serikali itutengee maeneo ya kutosha kuendesha shughuli zetu kwani mbali na kuwa sekta yetu ina mchango mkubwa kwenye uchumi wa Taifa lakini bado ushirikiano tunaopewa na taasisi za serikali hauridhishi," alisema Rehema.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti