• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mradi wa Maji Butimba kuwanufaisha zaidi ya wakazi laki nne Mwanza

Posted on: September 8th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Chanzo Kipya cha Maji eneo la Butimba kuongeza bidii ya ujenzi ili kukamilisha kwa wakati na uweze kuwanufaisha wananchi wanaosubiri mradi huo.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo leo Septemba 08, 2022 wakati akikagua mradi mkubwa wa cha Chanzo Kipya cha Maji eneo la Butimba unaosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa mazingira Mwanza (MWAUWASA) huku ukijengwa na Mkandarasi Kampuni ya M/S Sogea Satom kutoka Ufaransa kwa gharama ya Tshs. 69,337,520,300 ambao ulianza kutekelezwa Februari Mosi 2021 huku ukitarajiwa kukamilika Mwezi Februari 2023.

Aidha, amesema amefurahishwa sana na Utekelezaji wa mradi huo mkubwa na amewaagiza viongozi wa wilaya ya Nyamagana kuhakikisha utakapokamilika mradi huo wa maji uliofikia asilimia 40 ya utekelezaji kuhakikisha unawanufaisha wananchi wa eneo linalozunguka mradi huo kabla ya kusambaa kwenye maeneo mengine.

Mkurugenzi wa MWAUWASA, Mhandisi Leonard Msenyera amesema mradi huo mkubwa wa kisasa umegawanyika kwenye maeneo kadhaa yakiwemo Tanki kubwa, eneo la kuondoa madini tofauti, eneo la kubadilisha tabia ya maji, chemba ya kuondoa matope, eneo maalum la kuchuja maji, eneo la kuuwa wadudu na eneo la usafirishaji na kwamba hatua hizo zithakikisha ubora na usalama wa maji kuwa wa juu.

"Mradi huu wa Ujenzi wa Chanzo kipya na kituo cha kusafisha Maji safi cha Butimba utakapokamilika kwa awamu hii ya kwanza utazalisha lita elfu 48 kwa siku hivyo utaboreshwa huduma ya upatikanaji wa maji safi kwa wakazi wapatao 450,000 katika Jiji la Mwanza kutoka Nyegezi, Mkolani, Buhongwa, Lwamina, Fumagila, Sawha, Igoma, Kishiri na Nyamanoro, aidha maeneo ya Usagara, Nyashishi na Fella katika wilaya ya Misungwi na Kisesa, Bujora na Isangijo katika Wilaya ya Magu yatanufaika pia." Mhandisi Msenyera.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti