• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MTAKUWAA MWANZA YAWEZESHA KUPUNGUZA WATOTO WA MTAANI KWA 50%

Posted on: January 26th, 2026

Mkoa wa Mwanza kupitia Kamati ya Mkoa ya Usimamizi wa Utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) awamu ya pili (2024/25- 2028/29) umefanikisha kupunguza watoto waishio na kufanya kazi Mtaani katika kwa asilimia 50 hadi sasa.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Idara ya Mipango na Ufuatiliaji ya Mkoa huo Bw. Henry Mwaijega wakati akifungua kikao kazi cha kamati hiyo leo Januari 26, 2026 kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa huo chenye lengo la kupitia rasimu ya kitaifa na kutengeneza ya Mkoa.

Amesema tangu kamati hiyo izinduliwe mkoani humo imefanikisha Afua mbalimbali zikiwemo za watu wenye ulemavu na kufanikisha watu wenye ualbino 200 kupata vifaa saidizi na kujikinga na jua katika halmashauri za Misungwi na Kwimba vyenye thamani ya zaidi ya Milioni 200.

Aidha, amebainisha msaada mkubwa wa kamati hiyo katika kushughulikia Ukatili ambapo zaidi ya mashauri 250 yamefanyiwa kazi zitojanazo na Ukatili wa kijinsia, kutelekeza watoto na ukatili wa kingono katika kipindi cha julai -Desemba 2025.

Ameongeza kuwa wilayani Magu kamati hiyo kwa kushirikiana na viongozi wa halmashauri wamefanikisha kujenga kituo cha kushughulikia wahanga wa kijinsia (GBV One Stop Center) ambapo ni cha pili baada ya kile cha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou Toure.

Akihitimisha hotuba yake, Bwana Mwaijega ameendelea kuipongeza Kamati hiyo kwa kuwezesha mafunzo ya wataalam wakiwepo Jeshi la Polisi, Madaktari, Maafisa Ustawivwa jamii katika halmashauri ya Sengerema na kufanikisha usimamizi Shirikishi katika halmashauri za Kwimba na Buchosa.

Awali, akitoa utangulizi Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa huo Baraka Makona ametumia wasaa huo ku kuwapongeza Mashirika ya SOS Children Village na KIVULINI kwa kuwezesha uzinduzi wa Mpango wa Kutokomeza Ukatili kwa Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) mwezi Julai 2025.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti