• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mtihani wa kumaliza elimu ya msingi (PSLE 2019) kuanza kesho

Posted on: September 10th, 2019


Mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi kitaifa unatarajiwa kuanza hapo kesho tarehe 11 na kumalizika 12 septemba 2019, Mkoa wa Mwanza ni miongoni mwa mikoa iliyojiandaa vyema kuhakikisha mtihani huo unafanyika na kumalizika vizuri.

Akizungumza ofisini kwake Afisa elimu wa Mkoa wa Mwanza, Michael Ligola amebainisha kuwa jumla ya shule 949 kutoka mkoa wa Mwanza zinatarajia kufanya mtihani huo ambapo katika idadi hiyo shule 850 ni za mfumo wa Kiswahili na shule 99 ni za mfumo wa kiingereza.

Aidha Ligola amebainisha idadi ya wanafunzi wanaotarajiwa kufanya mtihani huo katika mkoa wa Mwanza wameandaliwa vizuri na wapo tayari kwa ajili ya mtihani huo hapo kesho.

“Mtihani huu unatarajiwa kufanywa na jumla ya idadi ya wanafunzi wapatao 68,078 ambao katika idadi hii wanafunzi 32,134 ni wavulana na 35,944 ni wasichana,” Alisema Ligola.

Ligola amebainisha kuwa idadi ya wanafunzi wenye uoni hafifu na wasioona watakao fanya mtihani huu kutoka shule za mfumo wa kiingereza na mfumo wa Kiswahili nao pia wameandaliwa vizuri na wapo tayari kufanya mtihani huo kwani hakuna changamoto zitakazokwamisha kufanikisha kwa mtihani huo.

“Mtihani huu utahusisha wanafunzi wasioona 7 ikiwa wavulana ni 6 na msichana 1 pia wanafunzi 37 wenye uoni hafifu kutoka shule za mfumo wa kiswahili ikiwa wavulana 14 na wasichana 13 na upande wa shule za mfumo wa kiingereza ni wanafunzi 5 kati yao mvulana ni 1na wasichana 4,” Alisema Ligola.

Hata hivyo Ligola ameaisitiza kuwa vifaa vyote vya mtihani vimeshawasili na wanafunzi wote wako tayari kwa ajili ya kufanya mtihani huo.

“Tayari tumepokea vifaa vyote na hatuna upungufu wa aina yoyote kwa upande wa watahiniwa pamoja na wasimamizi,”

Awali Ligola alianza kwa kuwatakia kheri wanafunzi wote watakao fanya mtihani huo wa kuhitimu darasa la saba na kuwatia moyo kuwa watafanya vyema na kuleta heshima katika mkoa wa mwanza.

 “Ninawatakia kila la kheri wanafunzi wote wa darasa la saba katika mtihani wenu wa kuhitimu elimu ya msingi na ninaimani mmejiandaa vyema katika mtihani wenu na ni matumaini yangu kuwa mtafaulu vizuri na kuleta heshima katika mkoa wetu,”

Pamoja na hayo Ligola amewaomba wazazi wa wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani wahakikishe wanafunzi hao wanafanya mtihani, pia ametoa onyo kwa wazazi wanaowashawishi watoto wao kufanya mtihani vibaya ili wasifaulu kuacha tabia hiyo, lakini pia amewataka wasimamizi kusimamia vizuri na kuacha udanganyifu katika mtihani ili kuweza kupata matokeo ya haki.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti