• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MUITIKIO MDOGO WA WANAFUNZI KURIPOTI SHULENI, RC MTANDA ATOA MAAGIZO

Posted on: January 20th, 2026

Halmashauri ya Wilaya Sengerema imepokea Tshs. Bilioni 2.16 katika mwaka wa fedha 2025/26 kwa ajili ya kujenga miradi 9 ya elimu zikiwemo shule mpya 4 fedha zilizokusudiwa kupunguza msongamano darasani na kuwapunguzia wanafunzi umbali wa kufuata elimu.

Akikagua miradi ya Elimu leo tarehe 20 Januari 2026 wilayani humo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka viongozi na watendaji wa halmashauri hiyo kuhamasisha wazazi na walezi wanawapeleka watoto shule katika ngazi zote kuanzia awali, msingi na kidato cha kwanza.

Mhe. Mtanda amewataka watendaji kuhakikisha wanapita nyumba kwa nyumba kuzungumza na wazazi na ili wawapeleke watoto shuleni huku akitolea mfano wa wanafunzi wa kidato cha kwanza kuwa ni asilimia 19 pekee (1561) ya walioandikishwa (7987) ndio wameripoti mpaka sasa.

Ameongeza kuwa wazazi wahamasishwe kuchangia mpango wa chakula shuleni ili wanafunzi wawe na nguvu ya kusoma na kupokea wanachofundishwa kwani wana uhakika wa chakula kilichozingatia lishe bora wakati wa masomo.

“Chakula kwa wanafunzi ni wajibu wa wazazi, hatuwezi kuwa na maendeleo mazuri kitaaluma ikiwa watoto wanashinda njaa shuleni hivyo twendeni tukahamasishe wazazi watoe michango halali iliyoidhinishwa na mamlaka.” Amesema Mhe. Mtanda

Akizungumza katika nyakati tofauti wakati akakikagua ujenzi wa shule mpya za Msingi Sima na Tabasamu Mhe. Mtanda ameagiza kasi ili kufanya ukamilishwaji wa haraka wa miradi yote hadi kufikia februari 28, 2026 ili wanafunzi wapate elimu katika miundombinu kamili.

Aidha, amewataka Wakala ya Maji vijijini (RUWASA) kuhakikisha wanapeleka huduma ya maji kwenye Taasisi na kwa wananchi wa Kata ya Sima kwani tayari serikali imejenga mradi mkubwa wa maji na kwa TARURA amewataka kurekebisha barabara ya kwenda kwenye shule mpya ya Tabasamu.

Akizungumza na wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha sita katika shule ya sekondari Mtunduru Mhe. Mtanda amewataka kusoma kwa bidii na kuacha kujihusisha na mapenzi wawapo shuleni na wazazi kuhakikisha wanawapa nafasi watoto wa kike kupata elimu kama wanavyopata wa kiume.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti