• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWANZA INA MAZINGIRA MAZURI YA KUWEKEZA KWENYE VIWANDA NA BIASHARA : RC MAKALLA

Posted on: November 24th, 2023

MWANZA INA MAZINGIRA MAZURI YA KUWEKEZA KWENYE VIWANDA NA BIASHARA : RC MAKALLA


*Abainisha kuwa Mkoa unaelimisha wananchi kujihusisha na Uvuvi wa kisasa*


*Asema Mkoa huo utaendelea kuimarika na kuchangia pato la Taifa*


*Asema kuwa miradi ya kimkakati itachochea biashara na kukuza uchumi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amebainisha kuwa Mkoa huo unaendelea kuweka mazingira mazuri ya kufanya uwekezaji na biashara ili wananchi wajishughulishe na shughuli za kiuchumi na kuweza kuinua pato la mtu mmoja mmoja na Taifa.

Makalla ameyasema hayo mapema leo Novemba 24, 2023 wakati akizungumza na Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo iliyopo Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Makalla amesema Mkoa huo upo kwenye zoezi kubwa la kutoa elimu kwa vijana ili waweze kujihusisha na uvuvi wa kisasa hususani kwenye vizimba jambo ambalo linahakikisha rasilimali za ziwani zinalindwa kwa manufaa ya muda mrefu.

"Kwa kuzingatia uwepo wa ziwa victoria, Mkoa wa Mwanza tunatoa elimu kwa wananchi kufanya uvuvi wa kisasa ambao ni wa kwenye vizimba na tunahamasisha wavuvi kuachana na uvuvi haramu", amefafanua.

Aidha, amebainisha kuwa uwepo wa miradi ya kimkakati inayoendelea kujengwa kama reli ya kisasa (SGR), Meli ya Kisasa ya MV Mwanza pamoja na Daraja la Kigongo-Busisi itasaidia sana kukuza biashara na kuchochea uchumi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mbunge wa Jimbo la Njombe Mhe. Deodatus Mwanyika amesema kuwa pamoja na kamati hiyo kusimamia fedha zinazopelekwa kwenye miradi inahamasisha pia uwekezaji kwenye viwanda ili kuongeza thamani ya malighafi.

Ndege ya mizigo ambayo Mhe. Rais ameinunua inaweza kuwa chachu ya kufufua viwanda kwani inatoa nafasi ya kusafirisha moja kwa moja malighafi kwenda viwandani kwa hiyo Serikali inahamasisha ufugaji, kilimo na biashara za kisasa ili kupata tija.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti