• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mwanza waja na kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa Msingi na Sekondari

Posted on: July 22nd, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amewataka Viongozi katika ngazi zote kuanzia kwenye Vitongoji kushirikiana kwa dhati kutekeleza Miradi ya Maendeleo kwenye maeneo yao shabaha ikiwa kuondoa changamoto zinazoikabili jamii.

Amesema hayo leo Julai 22, 2020 wakati wa Mkutano wa Wadau kuelekea Kampeni kubwa ya Ujenzi wa Miundombinu ya Vyumba vya Madarasa inayokwenda kuanza wiki ijayo Mkoani humo katika kuhakikisha wanafunzi kwenye shule za Msingi na Sekondari wanasoma kwenye madarasa bila kusongamana.

"Umoja ni nguvu, tunataka tuone kwenye majira haya ya mwanzo kabisa mwa mwaka wa fedha tunaazimia kwa pamoja kuwatoa watoto wa Shule za Msingi na Sekondari kwenye msongamano madarasani kwa kujenga vyumba vya madarasa vya kutosha." Amesisitiza.

Akifafanua suala la Elimu Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa huo kwa shule za Msingi una Mahitaji ya vyumba vya madarasa kwa zaidi ya elfu 18 na huku vilivyopo ni vyumba elfu 7 na kufanya kuwe na upungufu wa vyumba vya madarasa zaidi ya Elfu 11 ikiw ni sawa na asilimia 59 huku Halmashauri ya Nyamagana ikiongoza kwa upungufu.

Vilevile, amebainisha kuwa kwa Shule za Sekondari Mkoa huo una upungufu wa zaidi ya vyumba vya Madarasa zaidi 750 na kwamba hali hiyo imemfanya kuitisha Mkutano huo Mkubwa wa Wadau kuhakikisha wanaweka Mkakati wa pamoja ili kumaliza tatizo hilo mara moja.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Ndugu Ngusa Samike amebainisha kuwa Watendaji wote wako tayari kwa zoezi hilo nyeti na kwa hakika Mkoa unakwenda kulitekeleza kwa muamko mkubwa kwenye kila Halmashauri ili wanafunzi watakaoanza masomo mwakani watakupa mapinduzi makubwa sana kwenye suala la Miundombinu.

"Nikuhakikishie Mhe. Mkuu wa Mkoa kuwa Wabunge wote tumejipanga na tupo tayari kukuunga mkono kwenye kampeni hii, tutaenda kama timu na hakika Mwanza tunaanza safari hii leo na kwa hakika miezi sita baadae hatutakua sawa na sasa", amesema Mbunge Nyamagana, Mhe Stanslaus Mabula.

Mhe. Simon Mpandalume Diwani kutoka Magu ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) Mkoa amemshukuru Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa kuja na Kampeni hiyo na amemhakikishia kuwa Waheshimiwa Madiwani wapo tayari kushirikiana naye kwa dhati katika kufanikisha adhma hiyo ya kizalendo.

Mkutano huo umehudhuriwa na  Waheshimiwa Wabunge, Taasisi za kifedha, Kamati ya Amani, Mabenki, Marafiki wa Mkoa, Wachimbaji wa Wauza Madini pamoja na Waziri wa Maji (MB) Mhe. Jumaa Aweso ambaye yupo kwenye ziara ya kukagua Miradi ya Maji Mkoani humo na amechangia Mifuko 200 ya Saruji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti