• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWANZA YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA KUPITIA MAZOEZI YA PAMOJA

Posted on: January 21st, 2026

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Daniel Machunda ameongoza mazoezi ya pamoja kwa watumishi wa umma na wananchi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha jamii kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi ili kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza.

Mazoezi hayo yamefanyika katika Viwanja vya Furaisha Wilaya ya Ilemela, yakishirikisha viongozi mbalimbali wa serikali, vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi kutoka maeneo tofauti ya Jiji la Mwanza.

Akizungumza baada ya kuongoza mazoezi hayo, Bw. Machunda amewapongeza washiriki wote kwa kujitokeza kwa wingi na kuonesha moyo wa kujali afya zao.

Amewasisitiza wananchi na watumishi wa umma kuendelea kushiriki mazoezi mara kwa mara akibainisha kuwa mazoezi ni msingi muhimu wa afya bora na kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.

“Afya njema huanzia kwa mtu binafsi. Kufanya mazoezi mara kwa mara husaidia kuimarisha mwili, akili na kuongeza ufanisi kazini,” amesema Bw. Machunda.

Aidha, amewataka watumishi wa umma pamoja na wananchi kutoka taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kujitokeza kushiriki mazoezi ambayo hufanyika kila siku jioni kuanzia saa 12:00 katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Kwa upande wake, Afisa Mnadhimu Namba Moja Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi SACP Gideon Msuya amewapongeza washiriki kwa kujenga utamaduni wa mazoezi na kueleza kuwa shughuli hiyo imechangia kuimarisha ushirikiano, kutambuana baina ya taasisi mbalimbali pamoja na kubadilishana uzoefu wa kimazoezi.

Ameongeza kuwa mazoezi ya pamoja yanaimarisha mshikamano na mahusiano mema kati ya vyombo vya ulinzi na usalama na wananchi, jambo linalosaidia kudumisha amani na usalama katika jamii.

Mazoezi hayo ni sehemu ya mkakati wa Mkoa wa Mwanza wa kuhamasisha jamii kuzingatia afya bora kupitia mtindo wa maisha wenye mazoezi, lishe bora na kuepuka tabia hatarishi zinazochangia magonjwa yasiyoambukiza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti