• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWANZA YAPANDA ZAIDI YA MITI ELFU 16 MAADHIMISHO SIKU ZA KUZALIWA RAIS SAMIA

Posted on: January 27th, 2026

Mkoa wa Mwanza wametumia siku ya tarehe 27 Januari, 2026 ambayo ni Siku ya Kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupanda miti 16,000 katika maeneo mbalimbali ndani ya mkoa huo chini ya ushirikiano na Wakala wa Misitu nchini (TFS).

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Said Mtanda baada ya kushiriki zoezi la upandaji Miti zaidi ya 1200 katika Shule mpya ya Sekondari Kakebe- Igoma wilayani Nyamagana akiwa anahitimisha zoezi hilo aliloanza kwa kupanda Miti katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela.

Mhe. Mtanda amesema Mkoa wa Mwanza umeungana na Mhe. Rais kufanya kazi za kijamii kwa kupanda miti ya matunda ili kwenda sambamba na afua ya lishe bora wa watoto kwa siku za baadaye pamoja na kusaidia katika uhifadhi wa mazingira.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kupanda miti kwenye mashamba na hata katika mazingira ya makaazi ili si tu kupanda miti bali kufanya sadaka kwa Mwenyezi Mungu kwa kujenga taifa la kijani kwa siku za usoni.

“Suala la kuhifadhi mazingira ni la kizalendo, mazingira bora yatajenga maisha bora na jamii ikihifadhi vizuri tutapata mvua za kutosha hivyo niwatake wananchi wote kupanda miti kwenye kaya zenu,” amesema Mkuu wa Mkoa.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema pamoja kupanda miti katika Shule hiyo Wilaya imehamasisha upandaji miti katika maeneo yote hadi kwenye kaya na kwamba wanapanda miti ya matunda ili isiwe tu kwa ajili ya kivuli bali kuhamasisha lishe bora.

Aidha, ametumia wasaa huo kuishukuru Serikali kwa kuleta fedha nyingi za miradi huku akijinasibu kuwa upandaji miti kwenye shule hiyo mpya ya Kakebe utasaidia kuwaondolea wanafunzi adha ya kutembea zaidi ya Kilomita 5 kutoka Shamaliwa kwenda Igoma.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amechagiza hafla ya upandaji miti kwa kuendesha harambee kwa ajili ya kupata fedha Tshs. 1,800,000 za kuunganisha umeme na Maji kwenye shule hiyo ambapo zimepatikana Tshs. 1,350,800 papo hapo na amemuagiza Meneja wa TANESCO kupeleka umeme mara moja huku Maji yakifuata kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Jiji hilo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti