• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mwenge wa Uhuru kukimbizwa Mwanza kwenye Miradi ya Shs Bilioni 18.7

Posted on: July 13th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel leo tarehe 12 Julai, 2022 amepokea Mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Mwamhembo-Malya wilayani Kwimba ukitokea Mkoani Simiyu ambapo amesema utakimbizwa kwenye jumla ya KM 563 eneo la Nchi kavu na 'Nautical Miles' 86.3 eneo la Maji ziwa Victoria.

Aidha, amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Maendeleo Mkoani humo katika Sekta za Elimu, Afya, Miundombinu na Maji na amebainisha kuwa Mwenge wa Uhuru utaifikia Miradi 52 yenye thamani ya zaidi ya Tshs. Bilioni 18.7 kati ya hiyo 15 itawekewa mawe ya msingi, 29 itazinduliwa, 3 itafunguliwa na 5 itakaguliwa.

"Mwenge wa Uhuru utafanya ukaguzi kwenye miradi ya anuani za makazi inatotekelezwa katika Halmashauri zote ambapo hadi kufikia tarehe 7. 3. 2022 jumla ya nyumba 653,827 zimewekewa namba sawa na asilimia 118.54 hivyo kuvuka lengo lililowekwa. Jumla ya Anuani zilizosajiliwa katika mfumo ni 670,407 ambapo utekelezaji wa Mkoa umekamilika kwa asilimia 102." Amefafanua.

Vilevile, amesema zoezi la uwekaji Nguzo zinazoonesha majina ya Barabara limekua likiendelea vema Mkoani humo na kufikia tarehe 30 Juni, 2022 jumla ya Nguzo zilizotengenezwa ni 31,525 na kufanya Utekelezaji kukamilika kwa asilimia 104.7

Mhe. Mhandisi Gabriel amesema Mkoa huo umeendelea kutekeleza Kaulimbiu ya Mapambano dhidi ya Lishe duni, Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UKIMWI/VVU, na amebainisha kuwa yameendelea kupungua kutoka asilimia 15.1 hadi asimilia 8.1 mwaka hadi mwaka na kwamba vijana wameendelea kuwezeshwa kiuchumi kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Ndugu Sahil Nyanzabala ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha fedha wanazokopeshwa Vijana zinarejeshwa kwa wakati ili ziweze kukopeshwa tena kwa vikundi vingine na kuwasaidia kujikwamua kwenye shughuli mbalimbali kama za Kilimo, ujasiriamali, uvuvi, biashara na ufugaji.

Katika wakati mwingine, Mhe. Mkuu wa Mkoa amemkabidhi Mwenge wa Uhuru Mhe. Johari Samizi, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba utakaokimbizwa leo wilayani humo chini ya Kaulimbiu ya Kitaifa 2022 'Sensa ni Msingi wa Mpango wa Maendeleo, Shiriki kuhesabiwa tuyafikie Malengo ya Taifa'..

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti