• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MRADI WA MAJI YA BOMBA WA BILIONI 2.9 CHIFUNFU-SENGEREMA

Posted on: July 17th, 2023

MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MRADI WA MAJI YA BOMBA WA BILIONI 2.9 CHIFUNFU-SENGEREMA


Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye mradi mkubwa wa maji ya bomba katika kata ya Chifunfu-Sengerema unaotekelezwa na wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) kwa zaidi ya Bilioni 2.9 kutoka chanzo cha mfuko wa maji wa Taifa (NWT).

Akizungumza kwenye hafla hiyo leo Julai 17, 2023, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu Abdalla Shaib Kaim amewapongeza Mkuu wa Wilaya, RUWASA na watendaji wa Sengerema kwa ujumla kwa usimamizi mzuri ulioleta matokeo ya mradi bora unaoendana na thamani ya fedha zilizotumika.

"Mwenge wa Uhuru 2023 umekagua mradi huu kwa kina na itoshe tu kusema ubora umezingatiwa na hakika RUWASA mmeonesha nia ya kumuunga mkono Mhe. Rais kwa kumtua mama ndoo kichwani na kuwaletea huduma bora ya maji wananchi." amesema Ndugu Kaim.

Aidha, Ndugu Kaim ametoa wito kwa wakala huyo wa maji wa serikali kushirikiana na wananchi kuhakikisha wanapanda miti kwenye vyanzo vya maji na katika maeneo yote yanayozunguka miradi yao ili kuendelea kulinda na kuhifadhi vyanzo hivyo kwa vizazi vya sasa na baadaye.

Mhandisi George Genes Massawe

Meneja RUWASA Wilaya Sengerema amesema mradi huo mkubwa wa maji utainua hali ya upatikanaji maji safi na salama kwa wananchi 35343 kutoka vijiji vya Chifunfu, Nyakahako na Lukumbi kaya ya Chifunfu kutoka asilimia 6 hadi asilimia 88.9.

Mhandisi Massawe ameongeza kuwa mradi huo wenye vituo vya kuchotea maji 12 na tangi la ujazo wa lita laki 5 za maji utasaidia kupunguza magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa maji safi na salama kama kichocho, kuhara, tumbo, amiba na mengineyo.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mhe. Hamis Tabasamu (CCM) amebainisha kuwa Serikali imetekeleza mradi huo ikiwa ni katika adhma ya Serikali ya kuwaletea huduma safi za maji kama Ilani ya Chama cha Mapinduzi ilivyojibainisha wakati wa kampeni za Mwaka 2020 na kwamba haitaishia hapo bali wananchi hao wajiandae na mradi mkubwa wa barabara ili kuwapunguzia adha.


Vilevile, Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye shule ya Sekondari Ibondo na kuagiza madirisha na madawati yarekebishwe kutokana na kutengenezwa kwa gharama za wahandisi na mafundi kwani wametumia mbao mbichi na mkandarasi alipe kodi ya zuio kiasi cha Milioni 1.8

Mkopo wa Tshs. Milioni 8 walizokopeshwa Kikundi cha vijana wanaojihusisha na utengenezaji wa Samani katika mtaa wa Ibisabageni zimetosha kuwainua kiuchumi kwani wanazalisha na kuuza bidhaa hizo hata kufikia hatua ya Mwenge wa Uhuru kuwatembelea kabla ya kuzindua kituo cha mafuta 'Kwa Neema' kilichogharimu zaidi ya Milioni 400.


"Fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri Kiasi cha Shilingi Milioni 50 zimejenga madarasa mawili na kutengeneza madawati 40 ambapo zitasaidia kuondoa msongamano wa wanafunzi darasani na kuongeza kiwango cha ufaulu" amesema mwalimu Sundi Mussa wa Pambalu Shule ya msingi kwa niaba ya Mkurugenzi Sengerema wakati wa uzinduzi wa mradi huo.

Jengo la Wagonjwa wa Dharula linalojengwa kwenye Hospitali ya Wilaya hiyo kwa Shilingi Milioni 300 kutoka chanzo cha Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Udhibiti wa Ugonjwa wa Uviko 19 limewekewa jiwe la Msingi na Mkimbiza Mwenge ametoa wito kukamilishwa kwa haraka lakini kwa ubora unaotakiwa ili wananchi kutoka Kata 26 za Halmashauri hiyo na Halmashauri za jirani waweze kunufaika.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti