• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA KUKU WA MAYAI WA ZAIDI YA MILIONI 700 MISUNGWI

Posted on: July 18th, 2023

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA KUKU WA MAYAI WA ZAIDI YA MILIONI 700 MISUNGWI


Leo Julai 18, 2023 Mwenge wa Uhuru umezindua mradi wa ufugaji kuku wenye thamani ya zaidi ya Milioni 700 katika kijiji cha Idetemia Usagara Wilayani Misungwi ambazo kati ya fedha hizo asilimia 65 ni mkopo toka Benki ya Kilimo Tanzania (TADB).

Akizungumza kwenye uzinduzi huo, kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu Abdalla Shaibu Kaim amempongeza mwekezaji (Angroberg Farm Ltd) kwa uwekezaji huo mkubwa na wa kisasa ambapo hadi sasa mradi huo una jumla ya kuku 20,000.

Ndugu Kaim amesema, kuamua kuwekeza fedha kubwa kiasi hicho ni dalili ya kuwa imara kimaono na ubunifu na hasa baada ya kukagua na kugundua kuwa mradi huo umezingatia usalama, afya na utunzaji na uhifadhi wa mazingira.

"Huu si ufugaji tu bali ni wa kisasa, hongereni sana kwa ubunifu na uwekezaji mkubwa ambao umezingatia utunzaji na uhifadhi wa mazingira na kwa hakika Mwenge wa Uhuru umeridhika na ubora wa mradi." amesisitiza Ndugu Kaim.

Katika wakati mwingine Mwenge wa Uhuru umezindua madarasa aita kwenye shule ya Sekondari Idetemia yenye thamani ya zaidi ya Milioni 123 na kiongozi wa nbio za Mwenge wa Uhuru 2023 akatoa rai kwa Mkuu wa Wilaya hiyo kuongeza usimamizi kwenye miradi hususani eneo la manunuzi ya vifaa.


Aidha, kutokana na dosari zilizobainika kwenye mradi huo Ndugu Kaim ametoa siku nne kwa wilaya hiyo kuhakikisha wanazirekebisha ili kuhakikisha kunakua na ubora ili wanafunzi wapate mazingira wezeshi kwa kujifunza na kujifunzia na kuongeza ufaulu kwenye shule hiyo.

"Mhe. Mkuu wa Wilaya endelea kusimamia miradi yetu ili ikamilike kwenye ubora hususani kwenye upande wa manunuzi ya vifaa hakikisha bei zinazingatia nyaraka za vifaa vya ujenzi (BOQ) ili fedha zitumike vizuri," amesema Ndugu Kaim, kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2023.

Baada ya ukaguzi wa kikundi cha wasafirishaji abiria (Bodaboda) Ngudama-Bulemeji Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye jengo la mionzi kwenye kituo cha afya Misasi na kuagiza usimamizi mzuri ili hatimaye iweze kukamilika kwa wakati lakini kwa ubora madhubuti.

Mwenge wa Uhuru umeipongeza Halmashauri ya Misungwi kwa kubuni mradi wa vibanda vya biashara kwenye stendi ya mabasi vinavyojengwa kwa zaidi ya Milioni 75 ambapo mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi na kubainisha kuwa utasaidia kuongeza mapato ya ndani na kujihakikishia kujitegemea.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti