• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA UFUGAJI SAMAKI WA VIZIMBA NYAMAGANA

Posted on: October 9th, 2024

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA UFUGAJI SAMAKI WA VIZIMBA NYAMAGANA


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Godfrey Eliakim Mnzava amezindua mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba wa kikundi cha Vijana kinachojulikana kama Vijana Agro wenye thamani ya Tshs. Milioni 206 hadi kuanza uzalishaji.

Akizungumza na wananchi mara baada ya ukaguzi kwenye eneo la mradi huo uliopo katika mtaa wa Kisoko, kata ya Luchelele wilaya ya Nyamagana leo  Oktoba 09, 2024 Mnzava ameipongeza Halmashauri ya Jiji hilo kwa kuwakopesha vijana hao 7 kiasi cha tshs. milioni 150 hali iliyowafanya wapate na kupelekea kutengeneza miundombinu.

Aidha, amewataka vijana hao kuweka nidhamu kwenye utekelezaji wa mradi huo ili waendelee kuzalisha na kuuza samaki ambao soko lake ni kubwa sana kwa sasa na akawataka kuhakikisha wanafanya marejesho ya mkopo huo illi vijana na makundi mengine waweze kupata mkopo pia.

Akitoa taarifa ya mradi huo Mwenyekiti wa kikundi ndugu Christopher Gugu amesema mkopo huo pamoja na mtaji wao wa milioni 56 walizokua nazo hapo awali zimewasaidia kutengeneza vizimba 3 vikubwa, ununuzi wa boti na injini yake, mitumbwi 2, mashine 2 HP 15, tani 21.8 za chakula cha samaki, vifaranga pamoja na ujenzi wa stoo ya kuhifadhia chakula cha samaki.

Aidha, ametaja manufaa waliyoyapata kutokana na mradi huo kama kuongeza mapato ya kikundi kwani uvunaji wa awamu mbili na umewapatia milioni 86.4 na kuwafanya waanze kurejesha mkopo huo pamoja na kuongeza boti kutoka 3 hadi 6 na kwamba wameajiri vijana 6 nje ya vijana 7 waanzilishi.

Mwenge wa Uhuru Wilayani Nyamagana umetembelea mradi wa maji safi Butimba wenye thamani ya bilioni 71.9 unaotekelezwa na programu ya maji na Usafi wa mazingira ambapo baada ya ukaguzi kiongozi wa mbio hizo ameipongeza Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa mazingira (MWAUWASA) kwa kuongeza upatikanaji wa huduma hiyo kwa jamii.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti