• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

Posted on: January 23rd, 2026

Washiriki wa chuo cha taifa cha ulinzi leo Januari 23, 2026 wamehitimisha ziara ya mafunzo ya siku tano Mkoani Mwanza waliyoifanya katika maeneo mbalimbali mathalani kwenye miradi ya maendeleo ambayo wameitembelea kuona namna gani inatekelezwa.

Akizungumza kwenye hafla ya majumuisho Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameishukuru timu hiyo kwa ziara yenye tija ndani ya Mkoa na amewaahidi kufanyia kazi ushauri walioutoa katika kuboresha huduma.

Akizungumzia eneo la mipango miji, Mhe. Mtanda amebainisha mipango ya serikali ya kuwajengea wajasiriamali miundombinu rafiki ya kufanyia biashara ili wawe kwenye mazingira nadhifu na yenye tija kwao.

“Tutawasiliana na wizara ya Maliasili na Utaliii kuona namna ya kushirikiana nao kwenye kuongeza elimu kwa umma juu ya kutangaza vivutio vya utalii na kuweka mikakati ya kushirikiana na wadau kukuza sekta hiyo.” Mhe. Mtanda.

Naye, kiongozi wa timu hiyo Brigedia Jenerali Matunda amesema ziara yao imezaa matunda kwani wamepata walichokikusudia na wamejifunza mbinu, teknolojia na utekelezaji wa miradi kwa ujumla jinsi bavyo serikali inafanikisha.

Amesema, wamejionea kwa macho jinsi ambavyo serikali ya Tanzania imewekeza fedha nyingi kwenye miradi katika sekta za miundombinu, kilimo, utalii, uvuvi, ufugaji na viwanda jambo linaloipa nchi uhakika wa mazao na uzalishaji na kupelekea uhakika wa usalama wa chakula kwa wananchi wake.

Aidha, wameipongeza serikali kwa kuwajengea uwezo vijana kutumia mbinu za kisasa hususani kwenye ufugaji wa kisasa wa kuku na teknolojia ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba unaofanywa na makundi ya vijana ambao unasaidia kuhifadhi mazingira na kulinda mazalia ya samaki katika ziwa Victoria.

Pamoja na kupongeza kwenye uimarishaji wa usafiri katika ziwa kwa kujenga kituo cha uokozi na meli ya kisasa, wanafunzi hao wa vitendo wamebainisha changamoto kadhaa ikiwemo ukatishaji wa safari za ndege ambao wamehimiza kurekebishwa ili kutoikosesha serikali fedha kutokana na kodi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti