• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ONGEZENI BIDII DIMBANI ILI TUSHINDE MICHEZO MITATU ILIYOBAKI, EPUKENI HUJUMA: RC MTANDA

Posted on: April 12th, 2024

ONGEZENI BIDII DIMBANI ILI TUSHINDE MICHEZO MITATU ILIYOBAKI, EPUKENI HUJUMA: RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo amejumuika kwenye mazoezi ya timu ya Pamba Jiji FC kwenye uwanja mkongwe wa Nyamagana na kuwataka kukaza buti michezo yote mitatu iliyobaki ya ligi ya Championship na kuonya kusiwepo na aina yoyote ya usaliti kwa timu.

Mkuu huyo wa Mkoa aliyetinga uwanjani na kupasha mazoezi amesema michezo iliyobaki waipe uzito na kutoka na ushindi wa kishindo hasa kutokana na kupishana pointi chache na wanaonyemelea nafasi ya kupanda.

"Nawaahidi motisha zote zipo palepale alipoishia mtangulizi wangu mimi napaendeleza nimezungumza na uongozi wenu hivyo wajibu uliopo mbele yetu ni kushinda tu tukianzia mchezo wa kesho dhidi ya PGA Talent", RC Mtanda.

Aidha, Mtanda amewaonya wachezaji hao wasithubutu kujiingiza katika mchezo mchafu wa kuihujumu timu na atakayebainika hatosita kumchukulia hatua.

"Ni lazima mtambue tupo katika nafasi nzuri ya kupanda ligi kuu na pia mjihadhari na fitna zinazoweza kujitokeza ili tukwame katika malengo yetu," amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa aliyechezea timu ya Bunge.

Kocha Mkuu wa Pamba Jiji FC Mbwana Makatta amesema hana shaka na kikosi chake na kasoro zote za kiufundi zilizojitokeza wamezifanyia kazi.

"Mhe. Mkuu wa mkoa tumefarijika sana kuwa nawe na hasa kujumuika nasi katika mazoezi tumejiona ni mwenzetu haswa, sisi maelekezo yako yote tunayafanyia kazi ili tutimize ndoto ya kupanda ligi kuu msimu ujao,"Makatta

Mhe. Mtanda pia alitoa nafasi kwa mchezaji wa zamani wa timu hiyo Fumo Felician kutoa nasaha kwa wachezaji hao ambaye aliwakumbusha kutambua matarajio ya wana Mwanza ya kupata burudani ya ligi kuu kwa timu yao ya nyumbani waliyoikosa kwa miaka mingi.

Pamba Jiji FC maarufu kama TP Lindanda wakiwa na pointi 58 nafasi ya pili, watashuka dimbani Nyamagana Jumamosi hii kumenyana na PGA Talent kutoka Ruvuma kabla ya kufunga safari mkoani Arusha kuhitimisha michezo miwili na TMA Aprili 21 na siku saba baadaye dhidi ya Mbuni FC.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti