• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA AMEDHAMIRIA KUMALIZA KERO YA MAJI MWANZA : RC MAKALLA

Posted on: December 18th, 2023

RAIS SAMIA AMEDHAMIRIA KUMALIZA KERO YA MAJI MWANZA : RC MAKALLA


*Ampongeza Rais Samia kutoa fedha Bilioni 70 upanuzi chanzo cha maji Butimba*


*Ametoa fedha kupanua Chanzo cha maji Capripoint*


*Aelekeza ujenzi wa Matanki 5 makubwa uanze*


*Atinga Site kukagua ukarabati wa bomba lililoharibiwa na mvua Kishiri*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa chanzo cha maji Butimba uliokamilika Oktoba 30, 2023 ukijengwa kwa zaidi ya Bilioni 70 na kuzalisha Lita Milioni 48 kwa siku na akatumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha hizo.


Akizungumza leo kwenye chanzo cha mradi huo kilichopo kwenye kata ya Butimba Makalla amesema Mhe. Rais ameamua kwa dhati kumtua Mama ndoo kichwani kwa kumuondolea adha ya upatikanaji maji mkoani humo jambo ambalo awali lilikua ni kama ndoto kulifikia.

"Leo ni mara ya nne nimefika hapa ikiwa ni katika kusukuma ili mradi ukamilike, nawapongeza wote kuanzia Mkandarasi na viongozi kwa kutekeleza mradi huu ambao ni wa kisasa kabisa kwa jinsi mitambo niliyoiona ikifanya kazi, nachotaka sasa tuongeze nguvu kwenye ujenzi wa matanki na usambazaji," amesema Makalla.

Katika kuhitimisha ziara yake kwenye miradi ya maji Mwanza, Mkuu wa Mkoa amefika kweye mtaa wa Kishiri Bushitu kukagua ukarabati wa bomba lililoharibiwa na mvua na ameahidi kurekebisha hali hiyo mapema iwezekanavyo na akabainisha kuwa wananchi wa eneo hilo wanatarajiwa kujengewa barabara kwa kiwango cha lami KM 22 kutoka Buhongwa siku za usoni

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) Nelly Msuya amebainisha kuwa kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha si tu wananchi waliotajwa kwenye usanifu bali hata wengine nje ya mradi kwa kushirikiana na usambazaji wa maji yatokayo kwenye chanzo cha Capripoint.

Awali Mhandisi Selestine Mahubi ambaye ni Msimamizi wa mradi huo alifafanua kuwa wananchi wa mitaa ya Igoma, Kishiri, Ndose, Nyamaliwa, Nyamhongolo, Kisesa, Kanyama, Malimbe na Luchelele wananufaika na kwa upanuzi wa awamu ya pili watanufaika Usagara, Fela, Bukumbi, Nyashishi na Misungwi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti