• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA ANAWAPENDA WANANCHI WA KWIMBA AMEWALETEA MIRADI LUKUKI YA MAENDELEO : RC MAKALLA

Posted on: November 27th, 2023

RAIS SAMIA ANAWAPENDA WANANCHI WA KWIMBA AMEWALETEA MIRADI LUKUKI YA MAENDELEO : RC MAKALLA


*Ataja miradi wa ujenzi wa barabara kiwango cha lami Magu-Kwimba na Ngudu-Mabuki*


*Awataka watendaji Idara ya ardhi na wengine kuwasikiliza kwa staha na kutatua kero kwa wananchi*


*Asema Bilioni 1 imetolewa kujenga mradi wa maji Sumve*


*Awataka naafisa Ugani kutoa elimu ya kilimo bora kwa wananchi ili watumie mbegu na viuatilifu kwa wakati*


Leo tarehe 27 novemba 2023 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameshinda na wananchi kwa zaidi ya saa 10 kwenye Viwanja vya Stendi ya zamani Ngudu kusikiliza na kutatua kero zao huku akisisitiza kuwa atawasikiliza wote wenye changamoto bila kumuacha hata mmoja.

Akifungua mkutano wake Mhe. Makalla amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inawajali sana wananchi wa Kwimba kwani imeleta miradi lukuki ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa barabara ya lami ya Kwimba -Magu (Km 10).


Ameongeza kuwa pamoja na ujenzi wa barabara hiyo ambayo mkandarasi ameshapatikana, ameongeza kuwa Bilioni 1 imeletwa pia kujenga mradi wa maji kwenye jimbo la Sumve ambao umeshaanza kujengwa na umefikia asilimia 10 ya utekelezaji pamoja na miradi mingine mingi.


Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa ameonesha kutokua na imani na Mkandarasi anayejenga jengo la kisasa la Makao Makuu ya Halmashauri kutokana na kusuasua katika ujenzi wake pamoja na uwepo wa fedha za ujenzi ambazo ameshapatiwa na kumtaka kujitafakari kabla hajachukua maamuzi mengine.

Aidha, amewataka watendaji wa idara ya ardhi na wengine halmashauri hadi kwenye ngazi za vijiji kuwa na ratiba yenye tija ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi kwa wakati na kuhakikisha migogoro hususani ya ardhi inakomeshwa kwani kwa zaidi ya asilimia 80 ya kero zinazoibuliwa zimekua zikitoka kwenye sekta hiyo.

Halikadhalika, Mhe. Makalla awataka maafisa Ugani kutoa elimu ya kilimo bora kwa wananchi ili watumie mbegu na viuatilifu kwa wakati ili wapate tija na itaondoa tabia ya kulaumu serikali kuwa wanapewa mbegu, mbolea na viuatilifu feki wakati ni wao wanakosea wakati muafaka wa kutumia.


Awali Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija alifafanua kuwa amewasikiliza zaidi ya wananchi 400 na kwamba amebaini kuwa sekta ya ardhi imekua na migogoro zaidi hususani inayosababishwa na Mashamba ya urithi hivyo amewataka wananchi kufuata taratibu kwenye kuridhi mali ili kuepusha adha hizo na kwamba ofisi yake itaendelea na zoezi hilo.

Hata hivyo, Mhe. Ludugija ameahidi kuzifanyia kazi kero zote zilizoagizwa na Mkuu wa Mkoa ndani ya siku 14 na akawataka wananchi kutumia fursa zinazotolewa na serikali hususani wizara ya afya kupeleka watoto kwenye vituo cya kutolea huduma za afya kupata chanjo au dawa mbalimbali kwa ajili ya kuwakinga na kulinda afya za wananchi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti