• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Rais Samia atoa msaada wa chakula kwa vituo vya watoto waishio mazingira magumu Mwanza

Posted on: January 9th, 2024

Rais Samia atoa msaada wa chakula kwa vituo vya watoto waishio mazingira magumu Mwanza


Leo Januari 9, 2024 Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa msaada wa chakula kwa vituo viwili vya watoto waishio katika mazingira magumu na hatarishi Mkoani Mwanza katika wilaya za Nyamagana na Ilemela ikiwa ni zawadi za Sikukuu za Krismasi na na Mwaka Mpya.

Akikakabidhi zawadi hizo kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Daniel Machunda kwenye vituo vya Console kilichopo wilayani Nyamagana na Fonalisco kilichopo Ilemela kwa kila kituo ni mchele kilo 100,maharage kilo 100,mafuta lita 20,mbuzi 1,nyanya tenga 1,juice katoni 3 pamoja na biskuti maboksi 3 vyenye thamani ya Shs 1,700,000

Akizungumza na viongozi wa vituo hivyo pamoja na watoto hao Machunda amesema msaada huo wa Rais ni ishara ya kuendelea kuwakumbusha Serikali inawajali, inawathamini na kuwapenda hivyo wasijione wanyonge au kutengwa na jamii badala yake wadumu katika tabia njema na kuzingatia masomo ili waje kutimiza ndoto zao za kuwa viongozi au wafanyakazi bora wa Taifa hili siku za usoni.

"Nipo hapa mbele yenu kuja kuwaletea salamu za Rais wetu ninazo wasilisha mbele yenu kwa niaba ya mkuu wetu wa Mkoa Mhe.CPA.Amos Makalla amewasihi sana muishi kwa upendo huku mkiwa na imani Serikali ipo nyuma yenu kwa shida na raha hivyo ni wajibu wenu muendelee kujibidiisha katika masomo yenu kama anavyosisitiza Rais wetu kila mmoja asome bila kikwazo chochote,"amesisitiza Machunda wakati akizungumza na watoto hao kwenye kituo cha Fonalisco.

Amebainisha Ofisi ya mkuu wa Mkoa kupitia Idara zake husika itaendelea kuwa bega kwa bega na vituo hivyo kuhakikisha zinatimiza ipasavyo malengo yao ya kuwalea watoto hao kwa kuzingatia mila na desturi zetu ikitambuliwa hao ni hazina ya Taifa.

Kituo cha Console kilichopo wilayani Nyamagana kina  jumla ya watoto 17 na Fonalisco cha Ilemela kina watoto 101 huku baadhi yao wakiwa masomo ya elimu ya juu.

Rais Samia amekuwa na utaratibu wa kutoa zawadi  kwa watoto wote waishio katika mazingira magumu wakati wa sikukuu zote kubwa hapa nchini.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti