• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA AWEKEZA MIRADI MINGI YA MAJI NA AFYA KUWASAIDIA WANAWAKE NCHINI : RC MAKALLA

Posted on: March 8th, 2024

RAIS SAMIA AWEKEZA MIRADI MINGI YA MAJI NA AFYA KUWASAIDIA WANAWAKE NCHINI : RC MAKALLA


*Asema nchi imetulia, Rais Samia ni wa kuigwa kwa Demokrasia*


*Atoa wito kwa NGO's kuendelea kupinga ukatili wa kijinsia*


*Wanawake wakandarasi wapewe haki sawa kwenye kuteleza miradi*


*Madawati ya kupinga ukatili wa kijinsia kwenye maeneo yote yawepo*


*Maambukizi ya VVU yafikia 7.2 waathirika zaidi ni wanawake na wasichana*


*Mikopo ya Wanawake itarejea, Serikali inaandaa utaratibu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amesema kuwa upatikanaji wa maji mkoani Mwanza utafikia asilimia 86 kutoka 70 ya sasa vijijini ifikapo mwaka 2025 kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kwenye miradi ikiwa ni katika kuhakikisha wanawake wanaondolewa adha hiyo.

CPA Makalla amebainisha hayo leo, Machi 08, 2024 alipokua akihutubia wanawake wa Mkoa wa Mwanza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa kwenye viwanja vya Amani wilayani Misungwi.

Makalla amesema Rais Samia amekua akitoa fedha nyingi kwenye miradi mathalani zaidi ya Bilioni 30 kwenye mradi wa kata ya Kolomije wilayani Kwimba ambapo anakusudia kuwatua wanawake ndoo kichwani na akabainisha kuwa mikopo kwa Wanawake itarejea na sasa Serikali inaandaa utaratibu mzuri wa kutoa.

Aidha, ametoa wito kwa wakuu wa wilaya pamoja na asasi zisizo za kiserikali kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu ya madhara ya ukatili wa kijinsia kwa wananchi ili iwe na ufahamu na kuweza kujilinda na kuwa na ujasiri wa kuripoti waonapo madhila ya aina hiyo kwenye jamii.

Akizungumzia maambukizi ya virusi vya ukimwi yaliyofikia asilimia 7.2 amebainisha kuwa Mkoa huo unaendelea na mikakati ya kuondokana na madhila yanayopelekea maambukizi kuwa juu na akawataka wazazi kuzingatia malezi bora ya watoto kwenye kaya zao.


"Mkoa wetu una viongozi wanawake kwa ngazi mbalimbali mathalani Wakuu wa Wilaya watatu tena wanachapa kazi vizuri pia tunaye MNEC, mkurugenzi wa mamlaka ya maji ya mkoa tena amekua kinara katika kuendeleza mkakati wa kumtua mama ndoo kichwani." Makalla.



Akitoa salamu za wanawake mkoa wa Mwanza Mwenyekiti wa jamati ya maadhimisho hayo Zeyana Seif amesema ameiomba Serikali kuongeza shule za bweni kwenye shule za sekondari ili kundi hilo lipate mazingira mazuri ya kupata elimu na kupumzika badala ya kutembea umbali mrefu na kukutana na vishawishi.


"Ongezeko la watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, matumuzi ya dawa za kulevya, mimba za utotoni, ukatili pqmoja na watoto wa mtaani ni miongoni mwa matokeo ya wanawake kujikita kwenye utafutaji na kujihusisha na shughuli za uchumi hivyo tunaiomba Serikali irejeshe nfuko wa uwezeshaji kwa wanawake." Bi. Zeyana.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT) Mkoa wa Mwanza  Mhe. Adela Mayengela ametoa wito kwa wanawake kuisherehekea siku hiyo kwa dhati huku wakijiamini lakini akawakumbusha wajibu wa kuhakikisha wanachapa kazi ili kuliletea Taifa maendeleo na kumuunga mkono Rais Samia.


Jackline Aluta kutoka Shirika la Aman Girls Foundation amesema Shirika hilo kupitia mradi wa Afya, Elimu na uhifadhi wa jamii wanahakikisha wanawalinda mabinti kuanzia rika la umri balehe ili waweze kufikia ndoto zao kwa kupata elimu na sio kuingia kwenye masuala ya ngono.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti