• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAIS SAMIA AZINDUA MRADI WA MAJI BUTIMBA, ALETA KICHEKO KWA WANA MWANZA

Posted on: June 20th, 2025

RAIS SAMIA AZINDUA MRADI WA MAJI BUTIMBA, ALETA KICHEKO KWA WANA MWANZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo juni 20, 2025 amezindua mradi wa Maji na chanzo cha kutibu na kusafisha maji uliojengwa na Kampuni ya Sogea Satom na Vinci Grand Projects kutoka Ufaransa kwa thamani ya zaidi ya Tshs. Bilioni 70.


Akizungumza na wananchi katika hafla ya iliyofanyika katika viwanja vya mradi huo Butimba jijini Mwanza Mhe. Rais amesema mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha lita milioni 48 kwa siku utasaidia kuongeza mtandao wa usambazaji maji ndani na maeneo ya pembeni mwa jiji hilo takribani watu 450,000.


Aidha, amewapongeza MWAUWASA kwa usimamizi na amewashukuru wadau wa maendeleo waliotoa ruzuku na mikopo pamoja na Mkandarasi kwa ujenzi wa mradi huo na akawataka wananchi kulinda miundombinu ya mradi huo kwa manufaa ya vizazi vya sasa na baadaye.


Ameongeza kuwa miradi ya maji na usafi wa mazingira inayotekelezwa kila kona nchini imedhamiria kutegua kitendawili cha upatikanaji wa maji safi na salama na akawasihi wananchi kujenga uchumi wao kwa uvuvi na kilimo lakini wahakikishe wanahifadhi mazingira na vyanzo vya maji.


Naye, Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amebainisha kuwa awali mkoani wa Mwanza ulikua na chanzo kimoja tu kikubwa cha maji cha Capripoint ambacho kinazalisha lita milioni 90 kwa siku na kwamba kutokana na ongezeko la watu chanzo hicho kimekua finyu na ndipo serikali ikaamua kujenga chanzo kipya.


“Mhe. Rais, ilikuwa ni kitendawili kikubwa, wana mwanza wa Nyamagana na Ilemela walikuwa wanahoji kwanini ziwa lipo mwanza na wao wanakosa maji”, amesema Mhe. Aweso.

Mkuu wa Mkoa Mhe. Said Mtanda amesema mahitaji ya maji kwa sasa ni lita milioni 172 kwa siku huku vyanzo vya Capripoint na Butimba vikizalisha lita 138 na kwamba vimesaidia kuongeza kiwango  cha upatikanaji Maji kutoka 59% (2021) hadi 85% (2025) sawa na ongezeko la asilimia 25.


Aidha, amefafanua kuwa sekta ya maji Mkoani Mwanza imeimarika sana kwani kwa vijijini kupitia Wakala ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wametekeleza miradi zaidi ya 180 yenye thamani ya zaidi Bolioni 100.3 na hali ya upatikanaji imeongezeka hadi zaidi ya asilimia 78.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti