• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS BALANDYA AFANYA ZIARA YA GHAFLA KITUO CHA AFYA IGOMA, AWAPONGEZA WATUMISHI

Posted on: September 9th, 2024

RAS BALANDYA AFANYA ZIARA YA GHAFLA KITUO CHA AFYA IGOMA, AWAPONGEZA WATUMISHI

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana usiku wa Jumapili Septemba 8,2024 amefanya ziara ya ghafla kwenye kituo cha afya Igoma na kuridhishwa na utendaji kazi wa watumishi waliokuwa zamu muda huo na kuwataka kuongeza bidii ya kuwatumikia wateja wao.

Akiambatana na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Jesca Lebba,Balandya alianzia sehemu ya mapokezi ya wagonjwa kutoka nje OPD na kufanya mazungumzo nao namna walivyopokelewa na utaratibu mzima waliopatiwa kituoni hapo huku kila mteja akipongeza huduma sahihi walizopata.

Mtendaji huyo wa Mkoa alipita sehemu za wodini na wodi ya wazazi na huko pia alizungumza nao kabla ya kukagua sehemu ya kutolea dawa na kila eneo alishuhudia madaktari wa zamu na wasaidizi wao wakiendelea na kazi.

"Nawaombeni msiingie shaka kwa ujio huu na hasa kwa muda kama huu wa usiku, hii ni sehemu ya wajibu wetu kama viongozi na niwapongeze kwa kazi nzuri ya kuwahudumia wateja wenu,"amesema Balandya wakati akizungumza na watumishi wa kituo hicho na baadhi kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu.

Balandya amebainisha mara ya mwisho alipofanya ziara kwenye kituo hicho alipewa taarifa za changamoto mbalimbali za kiutendaji ukiwemo upungufu wa watumishi na uboreshaji wa mazingira ya kazi ambayvyo vyote vimefanyiwa kazi na mengineyo yapo mbioni kuboreshwa kulingana na bajeti ya Serikali.

Daktari wa zamu wodi ya wazazi,Mwita Chacha amesema wateja wake aliowapokea amawafanyia uchunguzi na wapo katika hali nzuri, na baadhi amewapa maelekezo ya kufanya mazoezi ili kurahisisha mzunguko wakati wa kujifungua

"Nampongeza Mganga Mkuu wa mkoa kwa kazi nzuri tangu umefika kituo chako kipya cha kazi hapa Mwanza sasa ni miezi miwili lakini umezunguka Halmashauri zote ili kujionea utendaji kazi na kutoa maelekezo," Balandya.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Jesca Lebba amesema yeye na timu ya wataalamu kutoka Ofisini kwake wameweka utaratibu wa kufanya ukaguzi na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa watumishi wa vituo na hospitali zote za Serikali ili kuhakikisha kunakuwa na muendelezo wa utolewaje mzuri wa huduma bora kwa wateja wao.

"Ndugu Katibu Tawala, Mkoa wetu umekuwa hauna rekodi nzuri katika uzazi wa mama mjamzito,tumejipanga vizuri kuhakikisha vifo vinatoweka kwa kiwango kikubwa kama ulivyojionea madaktari wa zamu wapo muda wote wodi ya wazazi na wote wamefanyiwa uchunguzi na wenye changamoto zimefanyiwa kazi ili wajifungue salama,"Dkt.Lebba

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti