• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS BALANDYA AWATAKA WATAALAMU WA MAABARA KUZINGATIA MISINGI YA TAALUMA

Posted on: September 25th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amewasihi wataalamu wa Maabara nchini kuhakikisha wanazingatia msingi na kuwa na weledi wa kitaalamu wanapofanya uchunguzi na vipimo ili kupata matokeo sahihi na kupelekea matibabu halisi kwa wagonjwa.

Ametoa wito huo leo tarehe 25 Septemba, 2025 wakati akifungua Mkutano wa 38 wa Jumuiya ya Wataalamu wa Sayansi Maabara (MeLSAT) kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya nchini uliowakutanisha wataalamu zaidi ya 600 kutoka ndani na nje ya nchi katika Ukumbi wa Kwa Tunza Beach uliopo Ilemela mkoani Mwanza.

Amesema, ni lazima wanataaluma wa Sayansi ya Maabara kuhakikisha wanazingatia sheria za taaluma zao na kukiepusha na matendo ya rushwa na ubatili mwingine wowote ili kuhakikisha majibu ya uchunguzi yanakua halisi na kuweza kutoa matibabu yanayostahili kwa wagonjwa.

“Maabara ndio uti wa mgongo wa matibabu kwasababu kabla ya mgonjwa kupata tiba ni lazima afanyiwe uchunguzi na vipimo ndipo abainike anaumwa nini na kupatiwa tiba hivyo nawasihi mhakikishe mnakua kiungo bora cha matibabu nchini ili tupate taifa lenye watu wenye afya nzuri.” Amesisitiza Katibu Tawala.

Aidha, ametoa wito kwa wataaluma wa maabara kujiunga na kuzingatia katiba yao katika kulipa ada na kuwa wanachama hai ili ikiwezekana wanachama wote elfu 16 wawe katika mwamvuli mmoja tofauti na ilivyo sasa ambapo ni elfu 6 pekee wamejiunga na akatoa rai kwao kushiriki kwenye makongamano.

“Wana taaluma wote wa maabara naomba niwasihi, kama mnataka kufika mbali kwa pamoja ni lazima muwe wengi na wamoja hivyo nawaombe mjiunge kwenye chama chenu (MeLSAT) na waajiri nchini muwawezeshe kushiriki katika vikao vya kitaaluma kuanzia kwenye uandaaji wa bajeti.” Amesema, Balandya.

Raisi wa Chama hicho cha MeLSAT Bw. Yahya Mnung’a amesema wanachama katika kongamano hilo pamoja na mambo mengine watajadili changamoto na mafanikio ya taaluma yao na matumizi ya akili unde na athari zinazoweza kuathiri taaluma hiyo na kuweka mikakati ya kukabiliana na matokeo hasi ya teknolojia hiyo.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti