• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RAS Mwanza awaahidi JWTZ Ushirikiano kwenye Miradi Mkoani humo.

Posted on: December 29th, 2023

RAS Mwanza awaahidi JWTZ Ushirikiano kwenye Miradi Mkoani humo


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana ameliahidi Jeshi la Wananchi nchini (JWTZ) kushirikiana nao kwenye Miradi mbalimbali ya kimkakati iliyopo mkoani humo ili iimarike kiulinzi na kiusalama kwa tija ya wananchi.

Mtendaji huyo wa Mkoa amezungumza hayo mapema leo Disemba 29, 2023 Ofisini kwake wakati wa mazungumzo mafupi na Meja Generali Shaaban Mani ambaye ni mkuu wa kamandi ya anga kutoka JWTZ, amesema kutokana na Teknolojia inavyozidi kushika kasi jeshi hilo lina umuhimu mkubwa kuhusishwa kwenye miradi hiyo ili nalo lijipange vizuri katika kutekeleza majukumu yake.

"Tuliona mwaka 1978 wakati wa vita dhidi ya Idd Amin Daraja la mto Kagera lilivyo shambuliwa na adui,hilo ni somo kwetu vikosi vya jeshi kuwa karibu na miundombinu kama hiyo," amefafanua Balandya wakati akizungumza na mgeni wake.

Balandya amebainisha Mwanza ina miradi mingi inayoendelea kujengewa kuanzia Reli ya kisasa,SGR,Daraja la JP Magufuli na Meli ya abiria Mv Mwanza na kituo cha kimataifa cha ulinzi na uokoaji Ziwa Victoria kilichopo mbioni kujengwa cha Jumuiya ya Afrika Mashariki ambacho makao makuu yake yatakuwa Mwanza,miradi yote hiyo watashirikiana na Jeshi ili izidi kuwa endelevu

"Sisi kama Jeshi ni wajibu wetu kuhakikisha muda wote Taifa lipo salama,nimefika Mwanza ili kukagua miundombinu yetu iliyopo chini ya kikosi cha anga na kama kuna changamoto ni kuzifanyia kazi haraka,"Mej Gen.Mani.

Katika mazungumzo hayo Mkuu huyo wa kikosi cha anga amemuomba Katibu Tawala wa Mkoa kuwapa maeneo yaliyovamiwa na wananchi ili waweze kufanya shughuli zao kwa ufanisi zaidi.

"Maeneo ya Jeshi ni lazima yawe mbali na makazi ya wananchi,kitendo cha nyumba za raia kuwa karibu yetu ni hatari pia kwa usalama wa nchi kwa mtu atakaye kuwa na nia mbaya,"amesisitiza Mej.Gen.Mani

Wakati huo huo Ndg.Balandya Elikana amemkaribisha rasmi Mkuu mpya wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza,Kamishna msaidizi,Kola Kayumba anayechukua nafasi ya mtangulizi wake Kamishna msaidizi Peter Mbaku anayehamia Mkoa wa Rukwa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti