• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Gabriel atoa Pikipiki 13 kwa RUWASA na vyombo vinavyotoa huduma za maji Mwanza

Posted on: June 29th, 2022


Leo Juni 29, 2022 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amekabidhi Pikipiki 13 zenye thamani ya Milioni 42.1 kwa Mameneja wa RUWASA Wilaya pamoja na kwa Vyombo vya Watoa huduma za Maji ngazi ya jamii (CBWSOs).

Akizungumza na wafanyakazi, wadau wa Maji na wananchi, Mkuu wa mkoa ametoa rai kwa RUWASA kukusanya Maduhuli ya Maji na kuhakikisha wanawafikia wateja kwa haraka na kutatua kero zao huku akibainisha kuwa kwa kufanya hivyo taasisi hiyo itasimamia vema Skimu na Miradi ya Maji na watatoa huduma bora kwa wananchi.

"Vyombo hivi lazima tuvitunze na kuhakikisha vinatumika kwa malengo kusudiwa pekee na Meneja RUWASA hakikisha zile Pikipiki 8 Mbovu zinakarabatiwa ili kukamilisha pikipiki 30 zinazotoa huduma kwenye uimarishaji wa huduma katika miradi yetu ya maji." Mhe Gabrie.


Aidha, ameagiza kuondolewa wakandarasi wanaokwamisha miradi ya maji ili dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kumtua Mama Ndoo iweze kutimia kwa upatikanaji wa Maji kwa urahisi kwenye jamii na ameahidi kuwa mkoa utafuatilia wabadhirifu watakaolenga kuhujumu miradi ya maji na watachukuliwa hatua.


Mhandisi Daud Amlima, Kaimu Meneja RUWASA Mkoa ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa kuwaletea vitendea kazi hivyo na amebainishaa kuwa pikipiki hizo zitakua Msaada mkubwa katika kuimarisha Miradi na skimu za Maji vijijini.

"Katika mwaka 2021/22 RUWASA Mkoa wa Mwanza imesaini Mikataba 51 yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 83 itakayohudumia zaidi ya watu 560,000 sawa na Asilimia 20 ya wananchi wanaoishi Vijiji, miradi hii itakapokamilika itafanya huduma za maji Vijijini kufikia asilimia 88" Mhandisi Amlima amefafanua.

Naye, Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Mwanza Mhe Ellen Bogohe, ameishukuru serikali kwa kuwa bega kwa bega na wananchi na kwamba uwepo wa pikipiki hizo umeitendea haki Ibara ya 100 ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwani zitaboresha Maisha ya wananchi Vijijini.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti