• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AONGOZA HARAMBEE YA KUICHANGIA PAMBA JIJI FC, ZAIDI YA MILIONI 177 ZAPATIKANA

Posted on: February 12th, 2024

RC MAKALLA AONGOZA HARAMBEE YA KUICHANGIA PAMBA JIJI FC, ZAIDI YA MILIONI 177 ZAPATIKANA


*Awashukuru wachangiaji kwa kufanikisha harambee*


*Ahimiza kuipa nguvu ya kiuchumi Pamba FC kwa kununua jezi kwa wingi*


*Awahakikishia wana Mwanza fedha zitakuwa salama*


*Abainisha Mkakati wa kuipandisha timu hiyo Ligi kuu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Februari 11, 2024 amewaongoza Wana Mwanza na wadau wa michezo katika harambee ya kuichangia timu ya soka ya Pamba Jiji FC na kufanikisha kukusanya jumla ya Shilongi milioni 177.3

Harambee hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mwanza Hotel michango hiyo imetoka kwa watu, taasisi mbalimbali za Serikali na watu binafsi wameitikia kwa wingi zoezi hilo lenye lengo la kuipa nguvu Pamba FC katika michezo yake ya Ligi ya Championship ili ipande kwenda Ligi kuu.

Katika hotuba yake ya kuwashukuru waliofanikisha harambee hiyo Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mlezi wa timu hiyo maarufu kama TP Lindanda amebainisha kuwa kupanda Ligi kuu siyo lele mama bali ni lazima kuwe na mikakati ya uhakika wa kifedha ambayo ndiyo chanzo cha mafanikio.

"Nilipoingia rasmi kama Mkuu wa Mkoa huu niliichunguza Pamba FC na kubaini inahitaji haraka nguvu ya kifedha, wameingia ndugu zetu wa NetSports hatuna budi kununua jezi kwa wingi ili kuzidi kuimarisha kiuchumi timu hii", CPA Makalla

Hotuba hiyo ya Mkuu wa Mkoa iliwaongezea hamasa washiriki wa harambee hiyo na kuzinunua kwa wingi jezi za Pamba Jiji wakiongizwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Mhe. Michael Masanja.

"Ndugu mgeni rasmi Mkuu wetu wa Mkoa hizi jitihada zako sisi kama viongozi wa soka Mkoa zinazidi kutupa ari kuwa mstari wa mbele kuipigania Pamba Jiji FC ili ifike malengo ya kupanda Ligi kuu msimu ujao," Vedasto Lugano M/kiti MZFA.

Meya wa Jiji la Mwanza ambaye ni wamiliki wa Pamba Jiji FC Mhe. Costantine Sima amebainisha watahakikisha nguvu hiyo ya wadau haipotei bure bali utakuja na matokeo chanya ambayo ni kucheza Ligi kuu msimu ujao.

Fedha hizo zilizotokana na harambee ni pamoja na michango taslimu ambayo ni zaidi ya Shilingi Milioni 28 na ahadi zaidi ya Shilingi milioni 100.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti