• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA APONGEZA UBORESHWAJI WA BANDARI NA KUWA MKOMBOZI KUPITIA MRADI WA SGR, MIZIGO MINGI KUFIKA KWA HARAKA MWANZA

Posted on: August 2nd, 2023

RC MAKALLA APONGEZA UBORESHWAJI WA BANDARI NA KUWA MKOMBOZI KUPITIA MRADI WA SGR, MIZIGO MINGI KUFIKA KWA HARAKA MWANZA


*Apongeza mpango wa uboreshwaji Bandari ya Dar utainua uchumi wa Mwanza kupitia mradi wa SGR


*Asema Fela ndiyo kituo Kikuu kitakachokuwa na shughuli nyingi za ushushaji mizigo na abiria,awataka wananchi kuchangamkia fursa za kiuchumi


*Awaondoa shaka wakazi wa kipande cha Fela kuja mjini fidia ya malipo yao kupisha mradi kulipwa mwezi huu


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA. Amos Makalla amepongeza uboreshwaji wa huduma ya Bandari ya Dar kuwa utainua uchumi wa Mkoa wa Mwanza kupitia mradi wa Treni iendayo kasi SGR kutokana na mizigo mingi kufika kwa haraka.

Akizungumza leo eneo la Fela na uongozi wa Kampuni ya CCECC pamoja na uongozi kutoka Wilaya ya Misungwi,.Mkuu huyo wa Mkoa amesema baada ya kupatiwa taarifa ya awali akiwa ofisini kuhusu mradi huo amelazimika kuja kujionea maendeleo yake na amefurahi kazi nzuri ya Mkandarasi huyo.

"Mwanza ni Mkoa uliokaa kimkakati uliopakana na nchi za Maziwa makuu, ujenzi wa reli hii na uboreshwaji wa Bandari yetu hii ina maana wafanyabiashara watanufaika na kufanya shughuli zao kwa uhakika kutokana na mizigo yao kufika kwa usalama na haraka",CPA Makalla

Amewataka wananchi wa  Mwanza na hasa wakazi wa Wilaya ya Misungwi kumuunga mkono Rais Samia Suluhu na mkakati wa kuiboresha Bandari kwani ni faida kwao kiuchumi mara mradi huo wa SGR utakapo kamilika

Aidha amempongeza mkandarasi huyo Kampuni ya CCECC kutoka China  kwa kazi nzuri ya kipande cha tano kutoka Isaka kuja Mwanza na ana imani hadi kufika Mei mwakani ujenzi huo utakuwa umekamilika.

"Huu mradi kutoka Isaka hadi Mwanza wa KM 341 umegharimu Shs Trilioni 3 ni fedha nyingi na tunamshukuru Rais wetu kwa ahadi aliyoitoa ya kuiendeleza kikamilifu miradi yote ya kimkakati iliyowachwa na mtangulizi wake wa awamu ya tano Hayati John Magufuli,"amesema CPA Makalla.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa mradi wetu wa kipande cha tano kutoka Isaka kuja Mwanza tunaendelea vizuri na tumefikia asilimia 35 hadi sasa, licha ya changamoto ndogo ndogo za kiujenzi kama kuhamisha udongo na kuweka mwingine utakaomudu uzito wa mataluma tunakuahidi hadi kufika Mei mwakani tutakuwa tumeukamilisha," amefafanua Mhandisi Christopher Kalisti,Meneja wa mradi

Akiwa njiani kukagua mradi huo wa SGR Mhe.Makalla amesimama eneo la Mkuyuni Tambukareli na kupata wasaa wa kuzungumza na wananchi ambao wametoa maeneo yao kupisha mradi huo na kuwaondoa shaka kuhusu malipo ya fidia zao ambayo yatafanywa mwezi huu baada ya taratibu zote za msingi kukamilika.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti