• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA ASHAURI TANROADS KUMUONDOA MKANDARASI WA BARABARA YA SENGEREMA- NYEHUNGE

Posted on: December 7th, 2023

RC MAKALLA ASHAURI TANROADS KUMUONDOA MKANDARASI WA BARABARA YA SENGEREMA- NYEHUNGE


*Amtaka TANROADS kumuondoa Mkandarasi anayejenga barabara hiyo na kumpata mwingine mara moja*


*Amempongeza Rais Samia kutoa fedha nyingi kwenye ujenzi wa Miundombinu mkoani humo*


*Amempongeza Mwenyekiti wa CCM kwa ushindi na amemuahidi ushirikiano wa Serikali*


*Awataka MaDC, MaDED,TANROADS na TARURA kudhibiti taka kwenye mitaro*


*Amewaelekeza Kamati za Usalama za Wilaya kwa kushirikiana na Kamati za Maafa kuwa tayari na majanga*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kumuondoa mkandarasi AVM Dillingham aliyepewa kazi ya ujenzi wa barabara ya lami ya Sengerema - Nyehunge (54.4KM) kwa zaidi ya Bilioni 73 kutokana na kuchelewa kuanza ujenzi huo tangia Mwezi Agosti na apatikane mkandarasi mweingine anapatikana na kuanza kazi mara moja.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa agizo hilo mapema leo tarehe 07, 2023 wakati wa Kikao cha kwanza cha Bodi ya Barabara Mkoa kwa Mwaka wa 2023/24 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mahususi kwa ajili ya kujadili maendeleo ya sekta hiyo.


"Mhe. Rais ametuletea fedha nyingi sana kutekeleza miradi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara ambayo nimeiona mwenyewe kwa macho nilipokua kwenye ziara ya kusikiliza kero, Mkandarasi wa ujenzi wa barabara ya Nyehunge- Sengerema kwa Bilioni 70 ameshapatikana lakini hajaanza kazi sasa naagiza TÀNROADS kumuondoa mara moja." Mkuu wa Mkoa.

Ameongeza pia miradi ya ujenzi wa barabara za Kayenze- Airport na Kwimba Magu ambazo zinaanza kujengwa kwa Kilomita 10 na Ngudu- Mabuki kwa Kilomita 3 pamoja na Bilioni 32 zilizotolewa kujenga vivuko vipya na kukarabati vya zamani sambamba na Bilioni 30 zilizotolewa za ujenzi wa Jengo la abiria katika kuufanya uwanja huo kuwa wa Kimataifa.


Vilevile, Mhe. Mkuu wa Mkoa Awataka TANROADS na TARURA kufanya usafi kwenye mitaro ili kuondoa takataka zinazozuia maji kutoririka vema kwenda ziwani ili kuweka hali ya usalama kwa kaya zisivamiwe na maji yanayotuama sehemu mbalimbali.

Kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini, CPA Makalla amezitaka kamati za usalama za Wilaya kwa kushirikiana na kamati za maafa kuwa tayari kukabiliana na majanga yanayoweza kutokea hususani Elnino kwani tayari mikakati ilishawekwa kwa usimamizi wake.


Aidha, Mkuu wa Mkoa amempongeza Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mwanza kwa ushindi wa kishindo alioupata kwenye Uchaguzi wa Chama hicho uliofanyika juma lililopita kufuatia kuhamishwa kwa mwenyekiti wa awali kwenda Masasi Mkoani Mtwara kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri.

Mhe. Michael Masanja, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza ametumia wasaa huo kuwashukuru wanachama wa chama hicho kwa kumchagua kwa kishindo kuwa Mwenyekiti kwenye uchaguzi na amewataka wadau wa sekta hiyo kuendelea kusimamia vema barabara na kulipa fidia kwa wakati kwenye miradi ya ujenzi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti