• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KWA JESHI LA POLISI MKOANI MWANZA

Posted on: August 2nd, 2023

RC MAKALLA ATOA MAAGIZO KWA JESHI LA POLISI MKOANI MWANZA


*Aagiza utoaji wa taarifa sahihi za uhalifu na wahalifu*


*Kutambua wageni wanaoingia na kutoka katika mitaa na kuwasajili*


*Atoa wito kwa Jamii kuacha vitendo vya kutembea na fedha nyingi*


*Ataka Ulinzi wa watoto uimarishwe kwenye jamii na kupinga natendo ya ukatili*


Leo Agosti 02, 2023 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amefungua Kikao Kazi cha Uelimishaji kwa Wakaguzi Kata, Watendaji na Wadau wengine kuhusu masuala ya Ulinzi na usalama chini ya Kamisheni ya Polisi Jamii nchini.

Akizungumza kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Mhe. Makalla amelitaka Jeshi hilo kushirikiana na viongozi wengine kama Mabalozi na Watendaji wa vijiji kutambua wageni wanaoingia na kutoka katika mitaa na kuwasajili ili kupunguza uhalifu.

Akisisitiza suala hilo Mhe. Makalla ametoa rai kwa Jeshi hilo kuhakikisha wanaendelea kuunganisha jamii na jeshi hilo katika kuhakikisha kila mmoja nchini anakua sehemu ya polisi jamii kwani wananchi ni muhimu sana kwenye masuala ya usalama.

Vilevile, amekemea tabia ya baadhi ya wananchi ya kutembea na fedha nyingi wakiona ni sifa, na badala yake amewataka kuweka fedha hizo Benki kwani wahalifu wanapata matamanio ya kufanya uhalifu wanapokua na taarifa za mtu fulani kutembea na fedha nyingi.

CPA Makalla ameagiza ushirikiano baina ya jeshi hilo na vyombo vingine ili kuhakikisha uhalifu unaondoka nchini na ametoa wito kwa Wakaguzi Kata kufanya kazi kwa weledi pasipo kuonea mtu kwa kushirikiana na viongozi wengine ili kuhimarisha usalama.

"Nafurahia kazi nzuri inayofanywa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, nakushukuru sana Kamishna wa Polisi Jamii kwa kuongoza kwa vitendo maana Maafisa Watendaji wa Kata kuwapo hapa leo ni ishara ya kufanya kazi kwa vitendo." Amesisitiza Mhe. Makalla baada ya kujinasibu kukomesha wizi wa vifaa kwenye mradi wa ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR).


Hata hivyo, ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kutoa taarifa za uongo za hali ya uhalifu na wahalifu na kuacha kufanya ramli chonganishi kwenye jamii pamoja na kuwalinda watoto na jamii kwa ujumla dhidi ya matendo ya Ukatili.


Naye Mkuu wa Kamisheni ya Polisi Jamii nchini, Kamishna Faustine Shilogile ametoa rai kwa watendaji kutoa ushirikino kwa Jeshi hilo ili kufanikisha lengo la dhana ya kuanzishwa kwa Kamisheni hiyo na amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuimarisha zaidi ulinzi kwenye maeneo yote.

Kikao Kazi hicho cha siku tatu kilichowakutanisha pia na wadau wengine kama mashirika yasiyo ya Kiserikali kinaongozwa na kauli mbiu isemayo 'Polisi Jamii kwa Usalama na Maendeleo yetu'.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti