• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AVALIA NJUGA KILIMO CHA PAMBA KUKUTANA NA MAAFISA UGANI WOTE KUPANGA MKAKATI WENYE TIJA

Posted on: December 8th, 2023

RC MAKALLA AVALIA NJUGA KILIMO CHA PAMBA KUKUTANA NA MAAFISA UGANI WOTE KUPANGA MKAKATI WENYE TIJA


 *Asema Pamba ndiyo zao la kuinua uchumi wa mkulima na Taifa*


*Kukutana na uongozi wa ATCL kuweka mkakati wa ndege ya mizigo iwanufaishe wafanyabiashara*


*Atangaza mpango wa kuinua ufaulu wa wanafunzi na kukomesha utoro shuleni*


*Maafisa ardhi awataka kutokaa ofisini na badala yake kwenda kutatua migigoro ya ardhi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla leo Disemba 8, 2023 amefungua kikao cha bodi ya ushauri wa Mkoa na kuweka bayana mikakati mbalimbali ya kimaendeleo likiwemo usimamizi wenye tija wa zao la Pamba kwa kukutana maafisa Ugani wote hivi karibuni.

Akizungumza na wajumbe wa kikao hicho kwenye ukumbi mkubwa wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Makalla amebainisha hakuna sababu ya zao la Pamba kuzorota wakati Serikali imeboresha kwa kiwango kikubwa sekta ya kilimo nchini.


"Wiki ijayo nitakutana na Maafisa Ugani wote kuanzia ngazi ya kata hadi juu, lengo tuone namna ya kulifanya zao hili liwe na tija kiuchumi kwa mkulima na Taifa kwa ujumla" CPA Makalla

Amesema Serikali imeweka mazingira rafiki kwa mkulima kwa kumpunguzia gharama za Pembejeo na kuboresha mbegu bora, hivyo ni wakati mwafaka kwa Mwanza kurudusha uzalishaji na kutoa Pamba itakayokidhi soko la kimataifa.


Kuhusu miradi ya maendeleo ya kimkakati Mkuu huyo wa Mkoa amewataka viongozi wote kutanguliza maslahi ya Taifa kwa kufanya usimamizi mzuri na hatimaye iwe na tija kwa manufaa ya wananchi.

"Rais wetu ametoa Shs bilioni 30 kwa ajili ya ukarabati wa uwanja wa ndege,wiki ijayo nikiwa na RAS tutakwenda kuonana na uongozi wa ATCL kwa lengo la ndege mpya ya mizigo iwanufaishe wafanyabiashara wa minofu ya samaki,nyama na mingineyo na hii ni baada ya kuvitembelea viwanda vyao na kusikia kilio chao katika usafirishaji,"amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa wakati anazungumza na wajumbe wa bodi ya ushauri wa mkoa


Kwa upande wa migigoro ya ardhi CPA Makalla amebainisha baada ya kuzunguka Wilaya zote za mkoa wa Mwanza amebaini kero nyingi zinatokana na watumishi kushindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo

"Kuna kiwanja kipo maeneo ya Liberty nimeamuru Halmashauri ya Jiji wamrudishie muhusika halali baada ya kubaini kuwepo na dhuluma ya waziwazi huu ni mfano mmojawapo ambayo ni mbaya kwa watendaji wetu,narudia kusema tukomeshe tatizo hili,"Mkuu wa Mkoa


Aidha CPA Mkalla yupo mbioni pia kukutana na Maafisa elimu wote kuweka kipaumbele cha kiwango cha ufaulu na kukomesha utoro shuleni.

Awali akitoa hotuba fupi,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Mhe.Michael Lushinge amesema kikao cha bodi ya ushauri wa mkoa ndiyo dira ya Mkoa kimaendeleo hivyo kuwataka wajumbe wote kwenda kuifanyia kazi mipango yote itakayowekwa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti