• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWAKARIBISHA INDONESIA KUWEKEZA MAZAO YA NGOZI NA MADINI

Posted on: February 26th, 2024

RC MAKALLA AWAKARIBISHA INDONESIA KUWEKEZA MAZAO YA NGOZI NA MADINI


*Asema Mwanza ina maeneo mengi yenye fursa za uwekezaji ukiwemo uvuvi


*Apongeza uhusiano wa Tanzania na Indonesia ulioanza tangu mwaka 1964


*Asema makubaliano ya mashirikiano yaliyofanywa na Marais yataongeza tija ya Maendeleo*


Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo amefanya mazungumzo mafupi na Balozi wa Indonesia hapa nchini Mhe.Tri Yogo Jatmiko na kutoa fursa ya kuwekeza katika mazao ya ngozi na madini yanayopatikana kwa wingi mkoani humo.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa yakijumuisha maafisa kutoka ubalozi huo na mwakilishi kutoka Wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mkuu huyo wa mkoa amesema makubaliano ya mashirikiano  yaliyofanywa na viongozi wa Mataifa hayo hivi karibuni ni lazima yawe na matokeo chanya kama uwekezaji huo.

"Mhe Rais wetu alifanya ziara hivi karibuni nchini Indonesia na kuingia makubaliano ya mashirikiano katika sekta mbalimbali kama elimu,kilimo,afya na biashara,lakini pia hapa mkoani kwetu zipo fursa nyingi ambazo zikipata mwekezaji zitakuwa na tija kwa wananchi wa pande zote mbili,"CPA Makalla

Amebainisha nchi ya Indonesia tuliyoingia nayo mahusiano tangu mwaka 1964 ni wazalishaji wakubwa wa mafuta ya mawese ambayo waliyatoa hapa nchini kwetu, wamewekeza zao la karafuu huko Zanzibar na sasa wanataka kujikita kwenye zao la Tangawizi,hii yote ni faida ya ushirikiano mzuri uliopo baina ya nchi hizo.

Aisha ameipongeza Indonesia kwa kuwajengea uwezo wataalam wa chuo cha DIT hali ambayo itaongeza tija Katika uzalishaji bora wa mazao ya ngozi.


Naye Balozi wa Indonesia Tri Yogo Jatmiko amesema anatekeleza na kuimarisha makubaliano yaliyowekwa baina ya nchi ya Indonesia na Tanzania katika sekta mbalimbali.

Indonesia imeanza kutoa mafunzo kwa wataalam wa ngozi kwenye chuo cha DIT kuanzia leo hadi Machi 8 2024 na mafunzo hayo yatakuwa yakifanyika kwa awamu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti