• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWAOMBA VIONGOZI WA DINI NA MILA KUELIMISHA JAMII KUEPUKA RAMLI CHONGANISHI

Posted on: June 1st, 2023

RC MAKALLA AWAOMBA VIONGOZI WA DINI NA MILA KUELIMISHA JAMII KUEPUKA  RAMLI CHONGANISHI


*Chanzo cha matukio ya mauaji yanasababishwa na ramli chonganishi Na imani Za kishirikina*


*Aagiza Watumishi kudumisha nidhamu mahala pa kazi*


*Atoa ratiba ya kusikiliza kero za wananchi kila wilaya*


*Amemshukuru Mhe. Rais kwa kuleta fedha nyingi za miradi ya Maendeleo*


*Asisitiza ukusanyaji Mapato na matumizi kwa mujibu wa sheria*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Amos Makalla ametoa rai kwa viongozi wa wilaya ya Magu kushirikiana naye katika kuwahudumia wananchi katika majukukumu ya kila siku.

Mhe. Makalla ametoa wito huo leo Juni Mosi, 2023 mbele ya viongozi, watendaji na makundi mbalimbali wilayani humo alipofika kwa ziara ya kikazi ya kujitambulisha.

"Hongereni Magu mmepata maendelo makubwa ukilinganisha na kipindi cha nyuma nilipofika hapa, napiga hodi Magu na nawaomba ushirikiano maana tuna majukumu mengi ya kufanya katika kuiinua zaidi Wilaya yetu." CPA Makalla.

Aidha, amewataka viongozi wa wilaya hiyo kuhakikisha kunakuwa na amani wakati wote huku akibainisha kuwa kuna viashiria vya uvunjifu wa amani kutokana na kuwa na historia ya matukio yanayosababishwa na ramli chonganishi.

"Imani za kishirikina kwa mfano kuamini unaweza kupata utajiri, mifugo au mazao mengi sana huku ukiwasikiliza waganga kuwa lete kiungo fulani hiyo si sawa na machifu mtusaidie kutoa Elimu kwamba hakuna njia ya mkato ya kuoata utajiri." Makalla.


Katika kusisitiza hilo, Mhe. Makala amewaagiza viongozi na watendaji wa ngazi za chini hususani kwenye vitongoji kuwa na ajenda ya kukemea masuala ya ushirikina kwenye vikao vyao vya kila wakati.

"Kila serikali ya kijiji muweke ajenda ya kutoa Elimu ya kuachana na imani za kishirikina na ramli chonganishi, tunataka wananchi wetu wawe salama na Polisi Jamii fanyeni kazi hiyo", Amesisitiza Mhe. Makalla.

Ameongeza kuwa pamoja na mafanikio makubwa waliyopata wana wajibu wa kufanya kazi kwa uadilifu hususani kukusanya mapato na kutumia kwa mujibu wa sheria ili kuepuka hoja za ukaguzi na kutoa tumaini kwa wananchi huku wakijibu kero zao.

"Nendeni mkajipange nitakuja kusikiliza kero za wananchi, anzeni kuweka mambo sawa hususani idara ya Ardhi, Maji, mifugo mimi sio mtu wa kukaa ofisini nitakuja kusikiliza kero za wananchi mbele yenu hapa na kitakua kipimo cha uwajibikaji wenu kama kweli mnawahudumia vizuri." CPA Makalla.


Vilevile, Mhe. Mkuu wa Mkoa ametumia wasaa huo kutoa pongezi na shukrani kwa Mhe. Rais kwa kupeleka fedha nyingi wikayani humo kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Maendeleo katika kila Sekta.

Katika wakati mwingine, Mhe. Makalla amekagua maendeleo ya Ujenzi wa jengo jipya la Kisasa la Makao Makuu ya Halmashauri hiyo na amewapongeza kwa usimamizi mzuri wa jengo hilo linalojumuisha Ofisi 72 pamoja na kumbi za Mikutano huki likigharimu Bilioni 5.7.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti