• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWAPANDISHA MZUKA PAMBA JIJI FC

Posted on: December 7th, 2023

RC MAKALLA  AWAPANDISHA MZUKA PAMBA JIJI FC


*Awamwagia noti wachezaji na benchi la ufundi kuelekea michezo miwili ya nyumbani*


*Awatia Shime mchezo dhidi ya TMA kutoka na ushindi nyumbani*


*Asema Pamba FC inastahili kukaa kwenye nafasi za juu katika msimamo wa Ligi ya Championship*


*Abainisha kuwaleta wachezaji  wanne kwa Majaribio kutoka Congo DRC kwenye Dirisha dogo la usajili*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Disemba 7,2023 ameitembelea kambi ya timu ya soka ya Pamba Jiji FC inayoshiriki Ligi ya Championship na kuwapa motisha ya Shilingi Milioni 4, ambapo 3 kwa wachezaji na 1 kwa benchi la ufundi kutokana na kuwa na matokeo mazuri katika michezo yao ya hivi karibuni.

Akizungumza na wachezaji hao iliyopo kambini hapo kwenye Mtaa wa Iseni nje kidogo ya Jiji la Mwanza, Mkuu huyo wa Mkoa amewapongeza wachezaji hao kwa kupambana vizuri dimbani na kushika nafasi ya tatu ikiwa na mtaji wa pointi 27.

"Kwa hadhi ya Pamba Jiji nafasi tuliyonayo ya pili nikiwa na maana Jumapili hii tunashinda na kushika nafasi hiyo ndiyo tunastahili na tusishuke bali tupande juu, "amefafanua Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mlezi wa timu hiyo.

Ameongeza kuwa wakati wa dirisha dogo atawaleta wachezaji wanne kutoka Congo DRC na kama dawati la ufundi litaridhika nao watasajiliwa kwa lengo la kuiongezea nguvu Pamba Jiji FC.

"Mhe Mkuu wa Mkoa tunaendelea kukuahidi kufanya vizuri katika michezo yetu na kutimiza lengo letu la kupanda Ligi kuu msimu ujao,tunakushukuru kwa kushikamana nasi,"Alhaji Majogolo,Mtendaji Mkuu wa Pamba Jiji FC.

Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA ndugu Peter Leti amesema kambi ya timu hiyo inaendelea vizuri na maelekezo yote anayotoa wanayazingatia hali ambayo yameleta matokeo chanya hadi sasa.

Nahodha wa wana TP Lindanda Jerryson Tegete akipokea kitita cha Shs milioni 3 kwa niaba ya wachezaji wanzake kutoka kwa mkuu wa Mkoa,amesema watazidisha ari ya kufanya vizuri ili kutimiza nia yao ya kucheza Ligi kuu.

"Mhe Mkuu wa Mkoa mchezo wetu dhidi ya TMA nakuahidi tutafanya vizuri kwani kasoro ndogo za kiufundi upande wa umaliziaji nimeufanyia kazi," Mbwana Makatta kocha mkuu wa Pamba Jiji FC.

Timu ya Pamba Jiji FC itashuka dimbani Nyamagana Jumapili hii kumenyana na TMA inayotokea Arusha.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti