• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA VETA KUWA NA KOZI RAFIKI KWA MAHITAJI YA WANANCHI WA KISIWA CHA UKEREWE

Posted on: November 23rd, 2023

RC MAKALLA AWATAKA VETA KUWA NA KOZI RAFIKI KWA MAHITAJI YA WANANCHI WA KISIWA CHA UKEREWE


*Amuagiza Afisa Elimu kuwajuza Wakuu wa Shule na Walimu wakuu kuhusu kuanza kwa masomo mwezi januari kwenye chuo hicho*


*Aagiza Baraza la Madiwani kushirikiana na kamati za maendeleo za kata kuhamasisha wananchi kupeleka vijana VETA*


*Amtaka Afisa Habari wa Halmashauri hiyo kupeleka matangazo redioni kuwajulisha wananchi uwepo wa chuo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ametoa rai kwa uongozi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) kuweka kozi fupi na zinazozingatia mahitaji ya eneo husika ili kuleta tija zaidi ya uwepo wa vyuo hivyo nchini kwa kupata vijana wengi zaidi kujifunza na kujiendeleza kwenye shughuli za kiuchumi.

Amesema hayo leo tarehe 23 Novemba, 2023 wakati akikagua ujenzi wa chuo cha Ufundi Stadi (VETA) kilichogharimu zaidi ya Bilioni 2.6 kwenye kijiji cha Muhula kwenye kisiwa cha Nansio wilayani Ukerewe huku kikitarajiwa kudahili zaidi ya wanafunzi 700 kwa wakati mmoja.


"Niwaombe uongozi wa VETA muwe na kozi zinazolenga mahitaji ya wananchi moja kwa moja, tunataka vijana wetu sasa wawe na ujuzi wa kutengeneza Boti na mbinu za kujihusisha na uvuvi wa kisasa ili watu wetu waweze kujiimarisha na kujiinua kiuchumi." Amesisitiza Makalla.

Aidha, amuagiza Afisa Elimu wa wilaya hiyo kuwajuza Wakuu wa Shule na Walimu wakuu kuhusu kuanza kwa masomo mwezi januari kwenye chuo hicho ili wawajuze wanafunzi wanaohitimu juu ya faida za uwepo wa fursa hiyo ambayo inawapa ujuzi wa vitendo moja kwa moja.


Vilevile, kupitia Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo ameliagiza Baraza la Madiwani kushirikiana na kamati za maendeleo za kata ili kuhamasisha wananchi kupeleka vijana kupata elimu ya Stadi za maisha ambapo itasaidia kufikisha elimu kwenye ngazi za chini hususani vitongojini na kwenye vijiji.

Katika kuhakikisha ujumbe wa uwepo wa fursa hiyo unafika kwa wananchi wote  wa wilaya hiyo yenye visiwa vidogo  38, Mhe. Makalla amemtaka Afisa Habari wa Halmashauri hiyo kupeleka matangazo kwenye redio hususani za kijamii zinazosikika visiwani humo kuwajulisha wananchi kwani njia hiyo itarahisisha kupeleka taarifa kwa haraka.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti