• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA WADAU WA MICHEZO MWANZA KUSHIRIKIANA KUPANDISHA TIMU LIGI KUU

Posted on: January 17th, 2024

RC MAKALLA AWATAKA WADAU WA MICHEZO MWANZA KUSHIRIKIANA KUPANDISHA TIMU LIGI KUU


*Asema Mpira hauna itikadi unawaleta watu pamoja*


*Asema mkakati ni Pamba Jiji ipande Ligi Kuu msimu huu, Mapinduzi FC ipande Championship*


*Alliance FC nayo isalie First League huku Copco ikipiganiwa isishuke daraja kutoka Championship*


*Aitisha hafla ya Kutunisha mfuko wa kusaidia timu zilizo katika ligi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoani humo (MZFA) kuimarisha ushirikiano na timu za mpira wa miguu zilizoko kwenye ligi mbalimbali ili zipande daraja.


Ametoa wito huo leo januari 17, 2024 katika mkutano wake na viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa huo pamoja na viongozi wa timu za Copco na Pamba Jiji zinazoshiriki Championship pamoja na Mapinduzi iliyo kwenye First League.

"Michezo ni uchumi, Mpira ni Uchumi kwani tukiwa na timu kwenye Ligi kuu basi Mkoa utafanya biashara mbalimbali hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na timu ya ligi kuu mkoani hapa na zingine kutoka madaraja ya chini zipande na kuja kwenye ligi za juu."

Makalla amesema kuwa michezo haina itikadi hivyo ni lazima wawe kitu kimoja katika kuhakikisha wanazipigania timu zote ili zipande kwenda ligi kuu na sio kuweka mahaba na ushabiki kwenye timu moja ambayo kwa muda mrefu imekua ikiugharimu mpira wa Mwanza.

Akizungumzia timu ya Pamba Jiji iliyoshuka kutoka Ligi Kuu mwaka 1992, amesema ni lazima ipande kutoka Championship ambapo wapo nafasi ya 2 kwa point 37 kwenda Ligi Kuu huku akitoa wito kwa Copco FC kuhakikisha wanabaki kwenye ligi hiyo halikadhalika Mapinduzi FC kuhakikisha wanapanda Championship kutoka First League ambako wako nafasi ya 1.

Aidha, ametumia wasaa huo kuwasihi wadau, makampuni na mashabiki wa mpira wa miguu mkoani humo kushirikiana kuhakikisha wanazisapoti timu zao kwa kuwatia moyo kwenye shida na raha hususani kwenye uwekezaji na sio kubaki wakilaumu tu wakati zinapofanya vibaya badala yake wawasapoti.

"Timu zote nawasihi tusiwe sehemu ya kuhujumiana badala yake tuwe kwa ajili ya kusaidiana, haifai kabisa ni lazima tuwe na uchungu wa kuhakikisha timu zetu zote Mkoa wa Mwanza zinapanda kutoka ligi ya chini kwenda ya juu hadi turudishe makali yetu Ligi kuu." Makalla.


Halikadhalika, Mkuu wa Mkoa ametoa kitita cha Milioni 6 yaani milioni 2 kwa kila timu katika kuwaunga mkono na kusaidia kushajihisha na kuwatia moyo kwenye safari yao ya kimpira inayoendelea ambazo amewataka wakazitumia katika kujikimu na mahitaji.


Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa huo Leonard Malongo ametumia wasaa huo kumhakikishia Mkuu wa Mkoa kushirikiana kubakikisha Mwanza inapata Timu kwenye Ligi kuu na kwamba watakua bega kwa bega kushirikiana na


Mwenyekiti wa Copco FC, Simon Romli amesema pamoja na mapambano mazito kwenye Ligi wao wanamshukuru sana Mkuu wa Mkoa kwa mchango na upendo wake kwa mpira wa Mwanza na ameahidi kuwa watahakikisha wanashirikiana kuhakikisha Mwanza inakua ni mkoa wa Mpira kwa kuwa na timu kwenye Ligi kuu.


"Hakuna siku ambayo sitaisahau kama siku uliyoangalia mpira wa timu yetu tukiwa tumekaa pamoja kwenye mawe, unajali unawiwa na unakiu ya kupata timu kwenye Ligi kuu, tunakushukuru sana Mhe. Mkuu wa Mkoa." Mwenyekiti wa Pamba Bhiku Kotecha.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti