• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO ZA WAFANYABIASHARA KABLA YA MWEZI DISEMBA KUISHA

Posted on: December 6th, 2023

RC MAKALLA AWATAKA WAKUU WA WILAYA KUSIKILIZA KERO ZA WAFANYABIASHARA KABLA YA MWEZI DISEMBA KUISHA


*Awaagiza Wakuu wa Wilaya kukutana na wafanyabiashara ndani ya mwezi Disemba kutatua kero zao*


*Awaagiza LATRA kuacha uzembe na kusimamia sheria za usafirishaji na siyo kupindisha*


*Awataka watendaji wa Serikali kubadilika, aagiza kuwahudumia wafanyabiashara kwa weledi*


*Awaagiza Halmashauri ya Jiji kummilikisha Z.E.K Landan kiwanja namba 1, Kitalu R mjini kati mara moja*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Wakuu wa wilaya mkoani humo kufanya mikutano ya kusikiliza na kutatua kero za wafanyabiashara kabla ya kuisha kwa mwezi Disemba mwaka huu ili kwa pamoja waweke uelewa wa pamoja wa namna ya kuboresha biashara zao.

Makalla ametoa agizo hilo leo Disemba 06, 2023 wakati akihitimisha kikao na Jumuiya za wafanyabiashara mkoani humo aliokutana nao kwa zaidi ya saa 5 kwenye ukumbi wa Mikutano mkoani hapo kuwasikiliza na kutatua kero zao ikiwa ni katika kuhakikisha wanaboresha biashara kwa pamoja.


Aidha, amewataka watendaji kila sekta kwenda kuangalia namna gani tozo zilizopo zinawaminya wafabyabiashara badala ya kuwainua zikiwa pia ushuru wa huduma ili kutoka na pendekezo la namna ya kuboresha na kuondoa sintofahamu hizo hususani utitiri wa tozo huku zingine zikionekana kujirudia baina ya taasisi.

"Watendaji wa mamlaka ya mapato na na maafisa biashara tuwe na lugha nzuri ya kudai kodi na kuwatia moyo watu ili wafanye biashara maana Serikali inaweka mipango mbalimbali ya kuboresha huduma za jamii kwa kutumia kodi hivyo ni lazima tutengeneze mahusiano mazuri na wafanya biashara na sio kuwakatisha tamaa."


Katika kushughulikia adhabu za makosa ya maegesho, Mkuu wa Mkoa ameagiza kuwekwa kwa vibao kuonesha sehemu zinazoruhusiwa na kukatazwa kwa wenye usafiri kuegesha badala ya kusubiri watumiaji wa barabara wafanye makosa ili wawatoze faini na pia akaagiza Jiji la Mwanza kumpatia haki yake Z.E.K Landan kwa kumnilikisha eneo lake lililopo mjini kati.

"Huu ni uzembe ni tabia ya watu kupindisha sheria, nataka operesheni ya kusimamia hatua hiyo ili daladala, bodaboda na bajaji zifuate taratibu zilizowekwa nawaagiza wakuu wa wilaya kwa kushirikiana na LATRA kwenda kushirikiana kuondoa changamoto" Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara, Mwenyekiti wa chemba hiyo Gabriel Chacha ametumia jukwaa hilo kuwasilisha kero 20 zinazowakabili huku zikijikita zaidi kwenye masuala ya utitiri wa Kodi, tozo, ushuru na leseni kinzani kwenye utoaji wa huduma na mamlaka za Serikali kuingiliana kwenye utozaji kwenye mambo yanayofanana.


"Sasa hivi kila mmoja ahakikishe anakwenda kwenye chuo cha mafunzo ya udereva asome apate cheti ndipo awe na sifa za kuwa na leseni na kuingia barabarani kuendesha gari, hii itasusaidia sana kuwa na usalama kuliko hali ilivyo sasa watu wana vyeti vya udereva bandia" Amesema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mtafungwa.


Mrakibu wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mwanza, SF Labani Kamila ametumia wasaa huo kuwataka wafanyabiashara kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo wanapokua na mipango ya ukaguzi wa stoo zao za bidhaa ili wawashauri namna nzuri ya kupanga ili kuepuka athari za moto na kuwa na vifaa vya kuzimia moto vinavyobebeka.


Naye Stella Marwa, Meneja Shirika la Bima la Taifa (NIC) kanda ya ziwa ametoa wito kwa wafanyabiashara kujisajili kwenye bima ili kujihakikishia ulinzi wa biashara zao wakati wa maafa kama moto kwani bima ipo kwa ajili ya kuwafanya wasipate hasara na sio kuwatia hasara.

Wakati huohuo, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Mwanza Mussa Mcholla amewasihi wafanyabiashara kutumia uwanja huo kusafirisha mizigo kwenda nchi mbalimbali duniani zikiwemo China na zote barani Afrika kwa kutumia shirika la ndege kwani Rais Samia amenunua ndege kubwa yenye tani 54.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti