• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWATAKA WANACHAMA WA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA NYANZA KUWA WAZALENDO NA KUJENGA USHIRIKA IMARA

Posted on: March 27th, 2024

RC MAKALLA AWATAKA WANACHAMA WA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA NYANZA KUWA WAZALENDO NA KUJENGA USHIRIKA IMARA


*Abainisha kurejeshwa kwa Akaunti Maalum (ESROW ACCOUNT) ya Chama Kikuu cha Ushirika NYANZA*


*Ataka kutumika vizuri kwa Akaunti hiyo katika kufufua Ushirika na kuleta tija*


*Ataka Chama kujipanga kushindana katika Soko na sio kukopa Wakulima*


*Awataka kuwa na mkakati wa kufufua viwanda vya kuchaka pamba*


*Awataka kusimamia upatikanaji na ugawaji wa pembejeo za Kilimo kwa wakati*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Chama kikuu cha Ushirika Nyanza kulinda Mali kwa uzalendo na kuwa na hatimiliki ili zisipotee badala yake ziendelezwe ili zizalishe Mapato na kuwa na Chama imara chenye Ushindani sokoni.

Mhe. Makalla ametoa neno hilo mapema leo Machi 27, 2024 wakati akifungua Kikao cha Siku moja cha Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama Kikuu cha Ushirika Nyanza (NCU- Nyanza Cooperative Union) kilichofanyika kwenye chuo cha Ualimu Butimba.

Amesema, katika kuimarisha Ushirika ni lazima kila mmoja kwenye umoja huo awe mzalendo katika kulinda mali na vitega uchumi za chama hicho kama Mashamba, Magari, Maghala, Nyumba, Viwanda n.k ili visaidie kukuza ushindani na kupanua biashara ili zisaidie kukuza uchumi wa chama hicho.

Aidha, amewataka kuhakikisha wanaboresha mnyororo wa thamani wa zao la Pamba kwa kufufua viwanda vya kuchambua pamba kwani kwa kufanya hivyo wataongeza thamani ya zao hilo, uhakika wa soko na kipato kwa wanachama wake na sio kukopa mazao kwa wakulima na baadae kutafuta masoko.

Vilevile, amewataka wanaushirika kusimamia upatikanaji na ugawaji wa pembejeo za Kilimo cha Pamba kwa wakati kwa wanachama wake, pia akawaagiza Maafisa Ugani kujiridhisha na takwimu za Mahitaji ya Pembejeo za wakulima wa pamba ili kuwezesha kuwa na takwimu sahihi za mahitaji ya pembejeo hizo kwa wakulima.

"Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC) imeanza kutumia mfumo wa TEHAMA, tunataka kuhakikisha wanachama wote wanajisajiri kwa 100% na kuzingatia matumizi ya miongozo 15 ya biashara ili kuendana kiushindani." Amesema Gabriel Mwita, Mwakilishi wa Mrajis wa Vyama vya Ushirika Nchini.

Vilevile, Mwakilishi huyo wa Mrajis amezungumzia uwekezaji unaotarajiwa kuanza rasmi mwezi Mei mwaka huu ambao utawafanya washirika kuwa na asilimia 51 za hisa ili waweze kuimiliki benki ya Ushirika na kwamba kwenye vyama vya ushirika kunakua na SACCOS ili kuinua mitaji ya wanachama.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti