• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI UKARA WA ZAIDI YA BILIONI 4.5

Posted on: November 22nd, 2023

RC MAKALLA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI UKARA WA ZAIDI YA BILIONI 4.5


*Amshukuru Rais Samia kwa kuwaletea wananchi wa kisiwa hicho maji safi*


*Mradi huo wafikia asilimia 80 ya utekelezaji*


*Aahidi kufuatulia fedha za ukamilishaji wa kradi huo*


*Awasihi wananchi kuutunza mradi kwa manufaa ya muda mrefu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Novemba 22, 2023 ameweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji Ukara unaotekelezwa na Mkandarasi M/S Halem Construction Company Limited kwa zaidi ya shs bilioni 4.5 chini ya usimamizi wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilaya ya Ukerewe.

Akizungumza na wananchi kwenye chanzo cha mradi huo Mhe. Makalla amemshukuru Rais Samia kwa kutenga fedha hizo kwa ajili ya kuwapatia maji safi wananchi zaidi ya elfu 40 wa kisiwani humo ambao wataondokana na adha ya kuugua magonjwa ya tumbo na hatari ya kuliwa na Mamba.

Makalla amesema nia ya dhati ya Rais Samia kwa wananchi wake wa vijiji vinane ni lazima itimie na kwenye hilo atahakikisha anafuatilia fedha za mradi huo ili mkandarasi aweze kulipwa na amemtaka kuendelea na kazi na kuhakikisha anakamilisha mradi huo muhimu kwa jamii.

"Niwahakikishie kwamba kazi hapa haita simama, ninakwenda kulifanyia kazi suala la fedha za mradi huu na mkandarasi abaki eneo lake la kazi aendelee kwani atakua shuhuda na wananchi wataona mabadiliko makubwa muda si mrefu." Makalla.

Aidha, ametumia wasaa kuwapongeza wabunifu wa mradi huo kwa kutumia nishati ya jua ambayo itasaidia kupunguza gharama za uendeshaji na amewasihi wananchi kulinda miundombinu ya mradi huo ili mradi wao uweze kujiendesha na kuwasaidia kwa muda mrefu.

"Kukamilika kwa mradi huu utakaosaidia wananchi kwenye vijiji 8 ni ishara ya kuondokana na maradhi ya tumbo na Rais Samia amedhamiria kuwafikia wananchi kwenye vijiji vyote 76 kwenye jimbo letu." Amezungumza Mhe. Joseph Mkundi Mbunge wa Ukerewe kwa niaba ya wananchi.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ukerewe Mhe. Ally Mambile amemshukuru Rais Samia kwa kuwajali wananchi wa vijiji vya Bwisya, Bukungu, Chifule, Chibasi, Nyang'ombe, Nyamanga, Kome na Bukiko na amebainisha kuwa Ilani ya chama hicho  anaitekeleza vema.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti