• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AZINDUA JENGO LA WAGONJWA WANAOHITAJI UANGALIZI MAALUM (ICU) BWISYA-UKARA

Posted on: November 22nd, 2023

RC MAKALLA AZINDUA JENGO LA WAGONJWA WANAOHITAJI UANGALIZI MAALUM (ICU) BWISYA-UKARA


*Lajengwa kwenye Hospitali yenye hadhi ya Wilaya Bwisya -Kisiwani Ukara*


*Awapongeza wasimamizi kwa kuokoa fedha zaidi ya Milioni 70 zilizojenga nyumba ya watumishi*


*Aagiza Ofisi ya Mganga Mkuu Mkoa kupanga ratiba za Madaktari bingwa kufika kwenye hospitali hiyo*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla, leo Novemba 22, 2023 amezindua jengo la wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum lililojengwa kwenye Hospitali ya Bwisya kwenye kisiwa cha Ukara kwa Shilingi Milioni 177 kati ya 250 zilizotengwa.

Akiongea na watumishi na wananchi, CPA Makalla ameipongeza halmashauri ya Ukerewe kwa usimamizi mzuri wa mradi uliopelekea kuokoa fedha zaidi ya Milioni 70 ambazo zimesaidia kujenga nyumba ya watumishi ya familia tatu kwenye hospitali hiyo baada ya kuongeza milioni 30 kutoka kwenye mapato ya ndani.

Mhe. Makalla amesema Rais Samia amewaletea huduma hiyo karibu kwa upendo wake kwani awali wananchi waliokua wakihitaji huduma hizo walilazimika kusafiri kwenda kwenye kisiwa cha Nansio wilayani Ukerewe jambo ambalo lilihatarisha afya zao.

"Nimezunguka ndani ya jengo hili (ICU) na nimeona limejengwa katika viwango bora na limewekewa vifaa vya kisasa kwa mahitaji ya kutibu wagonjwa watakaokua kwenye hali mahututi hivyo naomba mvitunze na kero ya watumishi wachache ninakwenda kulifuatilia", amesema Makalla.

Halikadhalika, ametumia hafla hiyo kumuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa kupanga ratiba za Madaktari bingwa kutoka kwenye hospitali ya rufaa ya Kanda Bugando kufika kwenye hospitali hiyo kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa kwa wagonjwa kwani jiografia inawapa ugumu kuzifuata jijini Mwanza.

"Uchache wenu (watumishi) usiwapelekee mkatoa huduma hafifu, tuendelee kuhudumia wananchi kwa upendo nami kwa nafasi yangu nitafuatilia suala la watumishi kuletwa hapa." Amesema Mhe. Joseph Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kwa niaba ya wananchi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti