• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AZINDUA KAMPENI CHANJO YA SURUA NA RUBELA, ZAIDI YA WATOTO LAKI 7 KUCHANJWA MWANZA

Posted on: February 9th, 2024

RC MAKALLA AZINDUA KAMPENI CHANJO YA SURUA NA RUBELA, ZAIDI YA WATOTO LAKI 7 KUCHANJWA MWANZA


*Ahimiza wananchi waelimishwe athari za Surua na Rubella na ni chanjo salama*


*Ataka Sekta zote zishirikiane na hamasa iwepo kutokomeza Kipindupindu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Februari 9, 2024 amezindua kampeni ya Chanjo ya Surua na Rubella kwa watoto wa miezi 9 na chini ya miaka 4 na miezi 11 itakayoanza Februari 15-18 ambapo zaidi ya watoto laki saba watapatiwa chanjo hiyo.

Akizungumza na wajumbe wa kamati ya afya kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Makalla amehimiza elimu na hamasa ya kutosha itolewe kwa wananchi kuhusiana na athari za ugonjwa huo na chanjo hiyo inayotolewa na Serikali ni salama na haina malipo.

"Bado kuna kasumba ya baadhi ya wananchi kukimbilia tiba mbadala badala ya kwenda vituo vya afya, nawaomba sana mjitahidi kutoa elimu ya kutosha ili mpango huu uwe na tija," amehimiza CPA Makalla.

Kuhusu ugonjwa wa Kipindupindu ambao amesema hadi sasa Mkoa wa Mwanza una wagonjwa 9, huku 7 wakitokea Sengerema na 2 wapo Ilemela,ametaka kuwepo na ushirikiano na hamasa kutoka Sekta zote ili kutokomeza ugonjwa huo.

"Mkakati wa elimu kuhusiana na ugonjwa huo tuendelee kutolewa ikiwemo kunawa kwa maji yanayotiririka, kuwa na choo bora na maji salama na kuepuka mazingira machafu yanayo tuzunguka,"Mkuu wa Mkoa.

"Niwaombe sana viongozi wa dini zoezi hili la chanjo muende mkatusaidie kuwaelimisha wananchi kujitokeza kwa wingi kuwapa chanjo watoto,lengo tufanikishe mpango huu,na kuhusu kipindu pindu mvua bado zipo maeneo yenye mlipuko hasa masoko na mialo miundombinu irekebishwe na usafi uzingatiwe",RAS Balandya.

Mganga mkuu wa mkoa wa Mwanza Dkt.Thomas Rutachunzibwa amewakumbisha watumishi wa Serikali kutoka sekta mbalimbali kuongeza juhudi ya kushirikiana na siyo kuiachia Idara ya afya pekee kupambana na ugonjwa huo.

Katika kampeni hiyo ya uzinduzi wa chanjo itakayoanza  imeambatana na utowaji wa elimu kuhusiana na ugonjwa wa Surua,Rubella na macho mekundu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti