• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MAKALLA AZITAKA HALMASHAURI KUWA NA MIPANGO INAYOJIBU KERO ZA WANANCHI MOJA KWA MOJA

Posted on: February 12th, 2024

RC MAKALLA AZITAKA HALMASHAURI KUWA NA MIPANGO INAYOJIBU KERO ZA WANANCHI MOJA KWA MOJA


*Asema ni lazima wananchi wasikilizwe na kutatuliwa shida zao*


*Ataka mipango ya kuongeza wigo wa Ukusanyaji wa Mapato*


*Aagiza udhiti wa Mapato kwa kusimamia mashine za kukusanyia mapato*


*Atangaza Mwezi Machi ni awamu ya usikilizaji kero Jimbo kwa Jimbo *


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza CPA Amos Makalla amezitaka Halmashauri kuwa na mipango madhubuti kwenye mpango wa Bajeti itakayojibu moja kwa moja shida za wananchi kupitia huduma zinazotolewa kwa jamii.

Ametoa wito huo mapema leo Februari 12, 2024 kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati akifungua kikao kazi kilichowakutanisha Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala, Wakurugenzi pamoja na Menejimenti za Halmashauri mahsusi  kujadili maandalizi ya mipango na Bajeti kwa Mwaka 2024/25.

Pamoja na Maagizo sita ya kufuata katika uandaaji wa Bajeti, CPA Makalla amesema ni lazima viongozi na watendaji wadumu kwenye kusikiliza kero za wananchi na kuziwekea mikakati ya kuzitatua mara moja kwani wananchi wengi wamekua na shida mbalimbali za kimaisha wanahitaji kusaidiwa.

"Nimefurahi kwamba nimepata majibu yaliyofanyiwa kazi kutoka kwenye kila wilaya kupitia ziara yangu niliyoifanya kwenye kila Wilaya, na ndio maana wamekuja viongozi wakuu wa nchi lakini hakukua na mabango ya malalamiko hiyo ni faida ya usikilizaji wa kero zao na kuzitatua." CPA Makalla.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa amefafanua kuwa katika kuhakikisha wananchi wanasikilizwa na kujibiwa vema kero zao ni vizuri wakapewa majibu kwa maandishi kwani inakua rahisi kwenye ufuatiliaji wa kero zao zilizobaki pamoja na kuweka kumbukumbu vizuri juu ya zoezi hilo.


Katibu Tawala Mkoa Balandya Elikana ametumia wasaa huo kuitaka Sekretarieti ya Mkoa na Menejimenti za Halmashauri na kuhakikisha katika upangaji wa Bajeti wanazingatia msingi unaoleta tija kwa wananchi wanaowatumikia pamoja na kuwa na vyanzo vipya vya mapato ili kupanua wigo wa ukusanyaji.


Aidha, amesisitiza kuzingatia mipango na mikakati ya udhibiti wa fedha za umma kwa kuzingatia matumizi sahihi ya mashine za mifumo pamoja na upelekaji wa fedha za mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo kwa mujibu wa sheria pamoja na usimamizi dhahiri wa miradi pamoja na upelekaji wa fedha kwa makundi maalum.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti