• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Malima ataka mashindano ya Mitumbwi yawe na sura ya kimataifa

Posted on: December 12th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewataka waratibu wa Mashindano ya Mitumbwi kuongeza ubunifu ktk mchezo huo ili kuwapatia washiriki bora watakaomudu ushindani wa kimataifa.

Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita Mwaloni Kirumba kwa niaba yake, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala amesema michezo ukiwemo huo wa Mitumbwi imekuwa nguzo imara ya ajira na kuwafanya wanamichezo kuwa na kipato kikubwa hivyo kuna kila sababu ya kuwajengea mazingira  ya kisasa wanamichezo hao kuwa wa kimataifa.

"Nawapa Rai waandaaji wa Mashindano haya ambayo yanafanyika kila mwaka hapa Mwanza,hawa wanazofanya vizuri wasiishie kuwapa zawadi ya pesa tu na kuja kuwatafuta mashindano yajayo hii ni sawa na kutoutendea haki mchezo huu na wachezaji husika Mhe.Masala.

Amesema mashindano haya sasa huu ni mwaka wa 14 tangu yaanzishwe,waandaaji sasa muone kuna kila sababu ya kuyatoa nje ya mipaka yetu ambapo huko hawa wachezaji watazidi kupata fursa ya ushindani wa juu na kupata timu za kulipwa ambayo ndiyo yawe malengo yetu na siyo kuishia hapa hapa tu.

Aidha amewapongeza waandaaji hao kwa kuzidi kuupa hamasa mchezo huo kiasi cha kuwa na mvuto kwa wakazi wa Mwanza na kutoa nafasi ya kuutangaza Mkoa huo Vivutio vingi vyenye fursa mbalimbali ikiwemo rasilimali ya maji ya Ziwa Victoria.

Naye msimamizi wa bodi ya Utalii Kanda ya Ziwa Gloria Muhambo amewahakikishia washiriki wa mchezo huo kuzidi kupewa ushirikiano kutokana na mashindano hayo kutoa ujumbe wa Vivutio vya Kitalii vilivyopo ndani ya Mkoa wa Mwanza.

"Tumeshuhudia uwezo mzuri wa kupiga makasia kwa washiriki wanaume na wanawake,naamini tutakapo wapa fursa ya ushiriki wa kimataifa Mkoa wetu utazidi kung'ara.

"Mkakati wetu sasa na kuyashirikisha Mataifa ya ukanda wa Maziwa Makuu kuwashindanisha wanamichezo wetu lengo likiwa ni kuwafungulia fursa za kuchomoza Kimataifa" Ludovick Kanyebuye mratibu wa mashindano ya mitumbwi Mkoa wa Mwanza.

Naye mratibu wa mashindano hayo kutoka Kampuni ya SCOPE inayosimamia mashindano hayo Benard Mweta amebainisha wamejipanga kuhakikisha mashindano yanakuwa bora na kuzidi kuviinua na kuvikuza vipaji vya washiriki ili waje kuwa washindani wa kimataifa

Katika mashindano hayo timu za kutoka Misungwi zimetoka kimaso maso kwa wanaume na wanawake kutokana na kushika nafasi za kwanza hadi tano,ambapo mahindi wa wanza amekunja kitita cha Shs milioni mbili,wa pili milioni moja na nusu,wa tatu milioni moja huku mshindi wa nne akitoka na laki 8 na wa tano akipata laki 5

Mashindano hayo yameshirikisha jumla ya timu 78,Wanawake wakiwa 18 kutoka Mara,Ukerewe,Misungwi na wenyeji Mwanza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti