• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Malima awataka TAMESA kusimamia ukarabati wa Vivuko kwa wakati

Posted on: December 19th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima kwa kupitia Kikao cha Bodi ya Barabara amewaagiza Wakala wa Umeme na Ufundi (TEMESA) kuhakikisha wanasimamia ukarabati wa Vivuko na Maegesho kwa wakati ili huduma hiyo muhimu kwa wananchi iweze kurejea kwenye ufanisi.

Akizungumza kwenye kikao hicho leo (Jumatatu Disemba 19, 2022) Mhe. Malima amesema Vivuko Mkoani humo sio anasa wala starehe bali ni huduma muhimu kwa wananchi kutokana na jografia ya uwepo wa makazi mengi kwenye Visiwa hivyo ni lazima kuwe na unyeti katika kuwahudumia.

Ameongeza kuwa vivuko 7 mpaka sasa vipo mikononi mwa Mkandarasi Songoro Marine chini ya usimamizi wa Wakala hiyo hali inayopelekea ugumu kwenye kutoa huduma  kwa wananchi kwenye maeneo mengi kwani ongezeko la abiria ni kubwa tofauti na vyombo vinavyotoa huduma.

Vilevile, amewataka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege kuboresha huduma kwenye uwanja wa Mwanza ikiwemo ukamilishaji wa jengo la kisasa la Abiria na upanuzi wa Barabara ya kutua ndege ili Uchumi ukue kupitia wageni watakaofika Kutalii kwenye hifadhi zinazozunguka kanda ya ziwa kama Serengeti, Burigi-Chato, Saanane, Kigosi na Rubondo.

Akizungumza kwa niaba ya TEMESA, Meneja Vivuko Kanda ya Ziwa na Magharibi Mhandisi Aloyce Ndunguru amefafanua kuwa Taasisi hiyo inaendelea kukarabati vivuko hususani MV Misungwi na maeneo ya maegesho na kwamba taratibu za Manunuzi ya vipuri zinaendelea kwa kushirikiana na Mkandarasi katika kuhakikisha wanakamilisha kazi.

Meneja Mradi kutoka Kampuni ya Songoro Marine William Basiga amesema pamoja na ucheleweshaji wa makabidhiano ya kazi na malipo, kampuni hiyo imejipanga kukamilisha Ukarabati wa vivuko hususani MV Misungwi ambapo tayari wameagiza injini zinazotarajiwa kuingia mwezi januari 2023 ili warejeshe huduma mara moja kwa wananchi.

Aidha, kikao hicho kimewataka pia Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) kufuta Ada ya Shilingi 400 wanayotozwa abiria kwa kuingia na kutoka kwenye kivuko cha Buchosa tofauti na ada ya kuvuka wanayotozwa kwani zinawaumiza wananchi kwa kubebeshwa mzigo.

Naye, Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa Mhandisi Paschal Ambroce amesema hali ya Mtandao wa Barabara kwa asilimia 21.7 ni nzuri hadi na kwamba jumla ya Tshs. Bilioni 16.7 zimetengwa kutengengeneza Kilomita 1,355.88 na Madaraja 5 ndani ya mwaka 2022/23.

"Katika mwaka wa fedha 2021/22 Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) tulikua na

jumla ya miradi 99 kati ya miradi hiyo 92 imekamilika na Miradi 7 ipo katika hatua za mwisho za utekelezaji kama miradi kiporo ambapo jumla ya Bilioni 27.23 zimetumika" Amesema Meneja wa TARURA Mkoa, Mhandisi Goodluck Mbanga.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti