• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC Malima awataka Ukerewe kuongeza kasi ya Miradi ya Maendeleo

Posted on: October 10th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Ukerewe amefanya Ziara ya Kikazi kisiwa cha Irugwa na Gana kukagua miradi ya maendeleo.

Akiwa Kisiwani Irugwa  ametembelea shule ya Sekondari  Irugwa ili kujionea miundombinu na hali halisi ya shule hiyo iliyokamilika ujenzi wa vyumba 6 vya madarasa 2021 vyenye thamani ya shilingi milioni 120.

Aidha, Mhe.Malima ameshiriki chakula cha mchana na wanafunzi wa shule hiyo ikiwa ni pamoja na kutoa zawadi ya shilingi laki tatu na thelathini (330,000) na kuahidi kuwapatia wanafunzi wa kidato cha nne Shilingi milioni 1 zitakazowasaidia kipindi cha mitihani, pamoja na Jezi za kiume na kike pamoja na mipira 2 kwa wasichana na 2 kwa wavulana.

Baada ya kukamilisha Ziara yake Kisiwa cha Irugwa Mhe.Malima na Kamati ya ulinzi na usalama alielekea Kisiwa cha Gana Kijiji cha Kamasi,Kata ya Ilangala na kukagua Ujenzi wa Zahanati na kuwapongeza wananchi kwa kuchangia Shughuli milioni 8 kwa ajili ya kununua eneo hilo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 60 na kuwataka waendelee kujitoa ili kufanikisha ujenzi huo.

Pamoja na wananchi kuonesha kuunga mkono juhudi za Serikali kuwasaida wananchi wake Mhe.Malima yeye binafsi amechangia ujenzi wa Zahanati hiyo shilingi milioni 1 pamoja na mfuko wa Mkuu wa Mkoa utachangia Shilingi milioni 1 na kuwataka wadau mbalimbali kuendelea kuchangia ili kufanikisha ujenzi huo.

"Serikali uwa inatoa milioni 50 pale ambapo kuna nguvu za wananchi zimeonekana, nendeni mkachangishane kuipa nguvu Serikali ya kuwashika mkono," amesema Mhe.Malima.

Hata hivyo,Mhe Malima ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kutatua Changamoto mbalimbali zinazokwamisha utekelezaji wa miradi katika Wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na maeneo hayo ya visiwani aliyoyatembelea bila kusahau upandaji wa miti ili kutunza mazingira.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti