• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

Posted on: June 17th, 2025

RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuzimaliza na kuzifunga hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambazo zimetokana na makosa madogo madogo kwa kurekebisha makosa yaliyofanyika ili kuzimaliza hoja hizo.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo juni 17, 2025 wakati akizungumza katika Baraza la Madiwani kuhusu hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza na kuwataka Maafisa Manunuzi na Maafisa Sheria wa Halmashauri kufanya kazi kwa pamoja katika kuzimaliza hoja hizo zilizojitokeza kutokana na makosa.

“Kama jambo lilifanywa au lilikosewa hata kama na watu waliopita kwa bahati mbaya na kupelekea kuibuka kwa hoja, ushauri wangu mliopo ni lazima kuhakikisha mnakaa chini mnaomba maoni ya CAG ya kuona namna ya kufuta hoja hizo”. Amesema Mkuu wa Mkoa.

Endapo nitaendelea kuwa Mkuu wa Mkoa huu wa Mwanza nikija tena katika Baraza la namna hii na nikakautana na hoja za namna hizi kwa kweli hatutaoneana muhali. Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Kuhusu hoja ya uwepo wa vyumba wazi katika Stendi ya Mabasi Nyegezi, Mkuu wa Mkoa ameitaka Menejimenti ya Jiji la Mwanza kuketi upya na kubadili mpango wa awali na kuja na mpango mpya unaoendana na uhalisia wa muktadha huo.

“Mimi nashauri ni bora kupata kidogo kuliko kukosa kabisa, kama vyumba vingine mlipanga kuweka hoteli na hamna mwekezaji aliyejitokeza msiendelee kusubiri badilisheni mpango” Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Halmashauri ya Jijij la Mwanza ilikuwa na Jumla ya Hoja 84, Kati ya hizo hoja za miaka ya nyuma zilikuwa 45 na hoja za mwaka wa fedha 2023/2024 zilikuwa 39. zilizofungwa baada ya uhakiki ni 35 hivyo hoja zilizobaki hadi sasa ni 49.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti