• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AAGIZA KUONGEZWA KWA VIFAA NA NGUVUKAZI KUKAMILISHA UJENZI KITUO CHA MICHEZO MALYA

Posted on: January 13th, 2025

RC MTANDA AAGIZA KUONGEZWA KWA VIFAA NA NGUVUKAZI KUKAMILISHA UJENZI KITUO CHA MICHEZO MALYA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka kampuni ya CRJE (East Africa) Limited inayojenga mradi wa kituo cha michezo cha umahiri Malya Wilayani Kwimba kuongeza nguvukazi na vifaa ili kuharakisha ujenzi huo.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo leo Januari 13, 2025 wakati alipofanya ziara chuoni hapo na kusema  Mkandarasi alipaswa kukamilisha mradi huo tarehe 16 mwezi huu kwa mujibu wa mkataba lakini ameshafanya kazi kwa asilimia 14.7 tu na kumpa onyo kwamba Serikali haitomvumilia endapo atachelewesha mradi huo.

Ameongeza kuwa, Serikali imetenga fedha zaidi ya Tshs. Bilioni 31 ili kuimarisha sekta hiyo nchini kwa kupata vifaa na miundombinu ya kisasa hivyo mkandarasi hatovumiliwa atapoonekana na lengo la kukwamisha juhudi hizo.

" Mkandarasi au mtu yeyote aliye hapa anaweza kujionea kwa macho ya kawaida tu kwamba vifaa na nguvukazi zilizopo hapa havioneshi dhamira ya kutaka kukamilisha mradi huu kwa haraka, sasa naagiza muongeze kabla sijawachukulia hatua."

Katika kufuatilia hilo kwa karibu, Mhe. Mtanda amemtaka mkandarasi kuketi pamoja na mshauri, uongozi wa Wilaya na chuo na kuwekeana ratiba ya kazi ambayo itafuatwa kila wakati na kuhakikisha wanaifuata na kuitekeleza.

Awali, msimamizi wa mradi huo mhandisi Feisal Msingwa alibainisha kuwa mkandarasi ameshalipwa malipo ya awali Tshs. Bilioni 3.1 na muda wa utekelezaji wa mradi huo ni mwaka mmoja (Miezi 12) kutoka Januari 2024 hadi Januari 2025 lakini alisimama kazi kwa muda wa miezi minne kutokana na ucheleweshaji wa malipo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti