• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

RC MTANDA AAHIDI KUTATUA KERO ZA WAUGUZI MWANZA, AWAHIMIZA KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Posted on: May 31st, 2024

RC MTANDA AAHIDI KUTATUA KERO ZA WAUGUZI MWANZA, AWAHIMIZA KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameungana na Wauguzi na Wakunga mkoani humo katika Kumbukizi ya mwanzilishi wa taaluma ya uuguzi Duniani, Florence Nightngale kwa kuwaahidi kutatua baadhi ya kero zao zikiwemo posho za sare za kazi na kupandishwa madaraja

Akizungumza na kada hiyo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure Mtanda amesema Serikali inatambua umuhimu na mchango wa wauguzi hivyo Ofisi yake itayafanyia kazi changamoto hizo.

"Mganga Mkuu wa Mkoa na wasaidizi wako nileteeni orodha ya watumishi wanaostahili  kupandishwa vyeo nitakaa na Katibu Tawala kulifanyia kazi na pamoja na hiyo posho ya sare 120,000 kwa mwaka.

Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha kuendelea kufanya kazi kwa weledi wakizingatia viapo vyao huku Serikali ikiendelea kuboresha mazingira yao ya kazi.

"Nimesikia katika risala yenu kuhusu upungufu wa watumishi kwa asilimia 40 hilo lipo kwa Serikali kuu na naamini litaendelea kufanyiwa kazi na Mamlaka husika"Mhe.Mtanda

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Thomas Rutachunzibwa amesema kwenye sekta ya afya bila wauguzi ni sawa na bure na siku zote wanaofanya kazi kwa zaidi ya uwezo wao,hivyo ni vyema wakapewa kipaumbele katika utatuzi wa changamoto zao ili kuwajengea ari ya kazi.

Kwa upande wake Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bi.Claudia Kaluli amesema licha ya uchache wao ambapo hadi sasa Mkoa una asilimia 60 ya wauguzi,wanaendelea kufanya kazi katika mazingira hayo wakiwa na matumaini ya hali hiyo kupatiwa ufumbuzi na Serikali.

"Ndugu mgeni rasmi siku hii hufanyika kila mwaka na sisi hapa Mwanza kuanzia Mei 29,2024 hadi leo tumefanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo upimaji wa Saratani ya shingo ya kizazi,magonjwa yasiyoambukiza pamoja na upimaji wa VVU na kutoa ushauri kwa wateja waliobainika na magonjwa husika na kuwapa ushauri wa kitabibu",Lucia Setembo,M/kiti wa chama cha wauguzi tawi la Seko Toure.

Siku ya Kumbukizi ya mwanzilishi wa taaluma ya uuguzi Duniani,Florence Nightngale imefanyika Kitaifa Mei 12,2024 .mkoani Tanga.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti